Jadon Sancho: Mchezaji wa kwanza wa Man U kutinga nusu fainali UCL tangu 2011

Katika kipindi cha miaka 13 iliyopita, Man Utd haijawahi vuka hatua ya robo fainali katika kinyang'anyiro cha ligi ya mabingwa na wana kila sababu ya kumhongera Sancho kwa kufika hatua hiyo, japo si kwa Man U bali Dortmund aliko mkoponi.

Muhtasari

• ESPN inaripoti kwamba maendeleo ya Dortmund yalimfanya Sancho kuwa mchezaji wa kwanza wa United kufuzu kwa nusu fainali ya Ligi ya Mabingwa tangu 2011.

• Mashetani Wekundu hawajavuka nane bora zaidi ya shindano la kiwango cha juu wa Uropa kwa miaka 13 iliyopita, na jaribio lao bora likiwa robo-fainali.

JADON SANCHO
JADON SANCHO
Image: x//ESPN UK

Jadon Sancho amekuwa mchezaji wa kwanza wa Manchester United kufika nusu fainali ya Ligi ya Mabingwa tangu 2011, kwa mujibu wa ESPN UK.

Nyota huyo wa Uingereza ambaye bado ana hali ngumu alikuwa sehemu ya kikosi cha Borussia Dortmund kilichojikatia tiketi ya kutinga hatua ya nne bora ya michuano hiyo Jumanne usiku.

Timu hiyo ya Ujerumani ilivuka baada ya kuifunga Atletico Madrid kwa jumla ya mabao 5-4 kwenye Uwanja wa Signal Park.

Wakiwa wamepoteza 2-1 katika mechi ya kwanza iliyochezwa Uhispania wiki iliyopita, Dortmund ilihitaji ushindi wowote nyumbani ili kusonga mbele.

Bao moja kutoka kwa Julian Brandt, Ian Maatsen, Niclas Fullkrug na Marcel Sabitzer lilifanya kazi ifanyike kwa wababe hao wa Bundesliga, huku Atletico wakiondoka kwenye dimba.

ESPN inaripoti kwamba maendeleo ya Dortmund yalimfanya Sancho kuwa mchezaji wa kwanza wa United kufuzu kwa nusu fainali ya Ligi ya Mabingwa tangu 2011.

Mashetani Wekundu hawajavuka nane bora zaidi ya shindano la kiwango cha juu wa Uropa kwa miaka 13 iliyopita, na jaribio lao bora likiwa robo-fainali.

Msimu huu, waliondolewa katika hatua ya makundi chini ya ukufunzi wa Erik ten Hag.

Kundi la United liliundwa na Bayern Munich, FC Copenhagen, na wababe wa Uturuki Galatasaray.

Winga huyo alitolewa nje kwa muda baada ya kutofautiana na Ten Hag mnamo Septemba 2023.