Messi aongoza Argentina kususia mechi kufuatia vita baina ya mashabiki wao na polisi wa Brazil (+video)

Mashabiki wa Brazil na Argentina waliaanza kupigana nyuma ya moja ya lango wakati wa wimbo wa taifa kabla ya polisi kuingilia kati.

Muhtasari

•Polisi wa Brazil ambao walikusudiwa kutuliza hali badala yake walizidisha mzozo huo baada ya kuanza kuwapiga mashabiki wa Argentina.

•Messi alikimbia hadi eneo la tukio katika juhudi za kutuliza hali kabla ya kuwaongoza wachezaji wenzake wa timu ya Argentina kutoka uwanjani.

Vita vilizuka wakati wa mechi ya Brazil vs Argentina
Image: HISANI

Mechi ya soka kati ya Brazil na Argentina usiku wa kuamkia Jumatano ilichelewa kwa takriban nusu saa baada ya kutokea mzozo mbaya kati ya mashabiki wa pande hizo mbili zilizochuana kwenye Uwanja wa Maracana mjini Rio de Janeiro, Brazil.

Polisi wa Brazil ambao walikusudiwa kutuliza hali badala yake walizidisha mzozo huo baada ya kuanza kuwapiga mashabiki wa Argentina ambao nao waliwashambulia na kusababisha mapambano makubwa ya ngumi, mateke na vipigo uwanjani.

Mashabiki wa Brazil na Argentina walikuwa wameanza kupigana nyuma ya moja ya lango wakati wa wimbo wa taifa, na kusababisha polisi wa Brazil kuwashtaki mashabiki wa ugenini kwa kuchomoa vijiti vya usiku. Baadhi ya mashabiki wa Argentina walijibu kwa kuwavamia na kuwarushia viti maafisa hao huku mashabiki waliokuwa wameingiwa na hofu wakiingia uwanjani kuepuka mapigano.

Picha na video zilizochukuliwa uwanjani wakati wa mzozo huo zinaonyesha shabiki mmoja wa Argentina akiwa amelala hoi uwanjani akiwa na uso uliojaa damu kabla ya kutolewa uwanjani kwa machela.

Baada ya kuona hali hiyo, mshindi wa Ballon d ‘Or 2023, Lionel Messi alikimbia hadi eneo la tukio katika juhudi za kutuliza hali hiyo kabla ya kuwaongoza wachezaji wenzake wa timu ya Argentina kutoka uwanjani kuandamana kilichotokea. Wachezaji walikaa kwenye chumba cha kubadilishia nguo hata baada ya muda uliopangwa wa mechi kuanza kufikika.

 Washindi hao wa kombe la dunia walirejea baada ya dakika 22 kwenye chumba cha kubadilishia nguo, na wakafanya mazoezi kwa dakika kadhaa kabla ya mchezo huo kuanza.

Mechi ilikuwa 0-0 hadi mapumziko kabla ya beki wa zamani wa Manchester City, Nicolas Otamendi kufunga katika dakika ya 63 na kuipa Argentina ushindi wa 0-1.

"Tuliona jinsi walivyokuwa wakipiga watu, tena kuwakandamiza watu, tayari ilitokea kwenye fainali ya Libertadores. Tulikwenda kwenye vyumba vya kubadilishia nguo kwa sababu ilikuwa njia bora ya kutuliza kila kitu, ingeweza kuishia kwa msiba," Messi alisema katika mahojiano baada ya mechi.

Wachezaji wa Argentina na mamlaka wameendelea kukashifu tukio hilo la kusikitisha lililotokea Jumanne usiku na wametaka kuwepo kwa mazingira ya amani zaidi wakati wa mechi.