NI KUBAYA! Viongozi wa tangatanga wafungiwa nje ya hafla ya Rais ,Nakuru (Picha).

Mbivu na Mbichi inaanza kubainika wazi pole pole katika siasa za uchaguzi wa mwaka wa 2022 na tayari tishio la rais Uhuru Kenyatta kwamba Viongozi wanaompinga watamtambua  yaonekana limeanza kutekelezwa .

Muda mdupi tu baada ya rais Kenyatta kumfuta kazi  Mwangi Kiunjuri ,waziri ambaye ameonekana wazi kuwa mfuasi wa karibu  wa naibu wa rais William Ruto katika baraza la mawaziri na kujihusisha sana na siasa za mwaka wa 2022  -Mwakilishi wa akina mama wa Nakuru Susan Kihika na  na Mbunge wa Nakuru Mashariki David  Gikaria wamefungiwa nje ya hafla ya kuwapa wakaazi wa Bahati  ,hati za kumiliki ardhi .Wawili hao waliarifiwa kwamba hawakuwa na idhini ya kuingia katika eneo la shughuli hiyo.