Afisa mkuu mtendaji wa shirika hilo Allan Kilavuka amesema maelekezo hayo yanaanza kutekelezwa julai tarehe 6 .
Kupitia taarifa kwa wafanyikazi wake KQ imewataka wale ambao huduma zao hazitahitajika kwa sababu hapatakuwa na shughuli nyingi za usafiri kuchukua likizo hiyo ya bila malipo kuanzia julai tarehe sita .
Amesema uamuzi huo umechukuliwa ili kuwapa fursa ya kuzungumza na washirika pamoja na wadau wengine kuamua hatua bora zaidi kwa wafanyikazi wa shirika hilo na kampuni nzima .
“ Ingawaje sote tumeweka juhudi kabambe za kuhakikisha kwamba tunaendelea na biashara yetu ,hali imekuwa ngumu na changamoto zilizopo ni nyingi kuendelea na oparesheni zetu’ amesema afisa huyo mkuu
Amesema tathmini yao imeeleza kwamba itawalazimu kupunguza idadi ya wafanyikazi hata wanapoanza kurejelea oparesheni baada ya sekta nzima ya usafiri wa angani kuvurusgwa pakubwa na janga la corona .
Kilavuka amesema kwa ajili ya uhaba wa watu wanaosafiri ndege zao nyingi zitasalia bila shughuli na hivo basi wafanyikazi wengi hawatahitajika .