Papa Shirandula alikuwa akinisaidia kusuluhisha migogoro na mke wangu asema Njoro

Mchekeshaji wa  kipindi cha Papa shirandula  Njoro kwa jina halisi  Ken Gichoya amezidi kufichua jinsi uhusiano wake wa karibu na  marehemu Charles Bukeko ulivyokuwa umenawiri kwa kiasi kwamba alikuwa jata akimsaidia kusuluhisha tofauti yake  Njoro na mkewe .

Njoro  ambaye alikuwa  akifanya kazi kwa karibu sana na marehemu Papa Shirandula amesema  kwamba  Papa hakuwa tu rafiki yake  bali alikuwa kama kakake mkubwa .

Akizungumza na katika kipindi cha Youtube cha Jalang’o  #BongaNaJalas,  Njoro amesema urafiki wa papa Shirandula ulikuwa nguzo muhimu sana katika shughuli zake kikazi na hata kifamilia akiwa nyumbani .

Amesema Papa alikuwa tayari wakati wote kutuliza mambo na kutafuta suluhisho wakati Njoro alipokuwa amejipata katika mgogoro na mkewe .

“Papa was not a friend to me he was a brother to me wakati nilikuwa na mashida nyumbani nilikuwa nikipigia Papa akuje aongee na bibi yangu mambo inakamilika. Papa alikuwa anasolve shida zangu za nyumbani,”  amesema Njoro

Njoro pia alisema walikuwa na uwekezaji pamoja na walikuwa wakisadiana kufungua biashara za wake zao .

“Second in terms of investments tulikuwa tunainvest na Papa tunaulizana sasa wife nikimuongezea hii project atakuwaje,”  aliongeza mchekeshaji huyo