Mkusanyiko wa Habari Muhimu Jumatano 9/10/2019

RADIO JAMBO MIC
RADIO JAMBO MIC

 OPARESHENI ya siku 11 ya  kuisaka miili ya mama na mwanawe waliozama katika bahari hindi huenda ikazaa matunda leo usiku au kesho asubuhi  baada ya wapiga mbizi kuona mabaki ya gari walilokuwa ndani .msemaji wa serikali Cyrus Oguna amesema kifaa hicho kimegunduliwa  kimo cha mita 58 chini ya bahari.

Bunge la kaunti  ya laikipia  limekuwa la 12 kuukata mswada wa punguza mizigo . waakilishi wa kaunti hiyo wamesema mswada huo wa muungano wa thirdaway alliance haujaafikiwa vigezo kadhaa ikiwemo kutohusishwa kwa wananchi kabla ya kuwasilishwa katika bunge hilo.

Huku hayoa yakiarifiwa  kiongozi wa thirdawya alliance Ekuru Aukot  amewashtumu wanasiasa kwa kujaribu kusambaratisha juhudi za kuupitisha mswada wa punguza mizigo  licha ya mswada huo kuendelea kukataliwa na mabunge ya kaunti . Aukot amesema wanasiasa wanawatumia wakenya na waakilishi wa kaunti kuukata mswada huo ili kulinda maslahi yao .

Iwapo unapanga kumtembelea rafiki au jamaa hapo kesho ,angalau hakikisha umabeba zawadi ya kumpa.mwanasosholjia Kennedy Ong’aro  anasema kumzuru mtu ukiwa mikono mitupu au na zawadi ya gmara ya chini ni jambo la kufedhehesha hasa iwapo hamjaonana kwa muda mrefu .

Mwanamme mmoja nahofiwa kuaga dunia baada ya shimo la choo alililokuwa akichimba kuporomoka na kumfunika katika kijiji cha marobo huko bungoma . shimo hilo la choo katika shule moja ya upili lilikuwa limefika kimo cha futi 25 .

Kando na wafanyikazi katika sekta ya kibinafsi  ,watumishi wa umma pia   wapo katika hatari ya kupoteza kazi zai kwani serikali ina mpango wa kupunguza idadi ya wafanyikazi wake katika siku chache zijazo . mtaalam wa masuala ya uchumi Charles karisa  amesema kampuni nyingi zinafungwa au kuwafuta kazi wafanyikazi kwa sababu ya gharama ya juu ya leba  na oparesheni hatua ambayo itaathiri  pato la jumla la nchi .

Gavana wa machakos Alfred Mutua  anataka waranti ya kuka,atwa kwake  iliyotolewa kwa kukaidi kufika mbele ya kamati moja ya senate kufutuliwa mbali . MuTUA ALIKATAA Kufika mbele ya kamati ya senate kuhusu  UHASIBU mara mbili akisema mazingira ya vikao hivyo hayakuwa salama .

Spika wa Nairobi Beatrice Elachi  amesalia afisini mwake licha ya kundi moja la waakilishi wa kaunti wanaompinga kujaribu kumfurusha .elachi  amemlaumu kiongozi wa walio wengi katika bung la kaunti  Abdi Guyo kwa masaibu yake .

Wanaharakati wa kutetea haki za binadamu wamewalaumu polisi kwa kutumia nguvu kupita kiasi wakati wa kuwakabili washukiwa waliomwua afisa mmja wa polisi  ambaye mwili wake ulipatikana siku ya jumamosi .Hussein Khalid  kutoka  haki Africa  badala yake amewarai polisi kutumia njia mbadala za kupata habari kutoka kwa wananchi   na sio kuwanyanyasa .

Wahudumu wa  matatu kutoka mlima Kenya wametishia  kulemaza huduma za usafiri  ili kulalamikia agizo la kuwataka  waweke vidhibiti mwndo vipya katika magari yao .wamesema agizo hilo la NTSA linawatwika mzigo wa gharama zaidi kwani hawakushauriana na NTSA kuhusu uamuzi huo wala kueleza kasoro za vidhibiti mwendo wanavyotumia sasa .

Polisi huko eldoret  wamewakamata washukiwa watano wa  wizi wa mifugo  na kupata mifugo waliobwa kutoka west pokot .kamanda wa polisi katika kaunti hiyo johnstone ipara  amesema washukiwa hao ni pamoja na afisa mmoja wa zamani wa KDF  ilhali washukiwa watatu walitoroka .

Maafisa wa polisi nchini Uganda wamefutilia mbali tamasha la mbunge wa Kyadondo mashariki Robert Kyagulani maarufu Bobi Wine lililotarajiwa kufanyika karibu na mji mkuu wa Kampala.Naibu inspekta jenerali wa polisi Asuman Mugyenyi anasema kwamba waandalizi wa tamasha hilo walishindwa kuweka usalama uliohitajika, kulingana na chombo cha habari cha Nile Post.