Mkusanyiko wa Habari na Matukio Muhimu Ijumaa 11/10/2019

RADIO JAMBO MIC
RADIO JAMBO MIC
 Peter Karanja,  Mtuhumiwa wa pili katika mauaji ya mdachi Tobe Cohen  amekanusha mashtaka ya  mauaji dhidi yake .karanja  amejibu shtaka hilo mapema leo baada  ya mahakama kuthibitisha kwamba yuko timamu  kufika kortini ili kujibu mashtaka .ombi lake la kutaka kuachiliwa kwa dhamana  litasikizwa alhamisi wiki ijayo .

Rais Uhuru Kenyatta ametuma ujumbe wa kumpongeza waziri mkuu wa Ethiopia Ahmed Abiy kwa kushinda tuzo  ya amani ya Nobem mwaka huu . Abiy ametangazwa mshindi wa tuzo hiyo hivi  leo kwa ajili ya juhudi zake kuleta maafikiano kati ya nchi yake na Eritrea ambazo zimekuwa zikizozana kuhusu mpaka kwa miaka 20.

Katika saa 17 zijazo  mwanariadha bora wa mbio za marathon  Eliuv Kipchoge  atafanya jaribio la kihistoria la kukimbia mbizo za kilomita 42 chini ya saa mbili ili kudhihirisha kwamba  binadamu anaweza kuafikia lolote bila vikwazo . mshikilizi  huyo wa rekodi ya dunia  anataka kuweka rekodi mpya ya saa moja na sekunde 59 katika mbio za INEOS 159  hapo kesho huko vienna Austria .

MAHAKAMA Kuu imefutilia mbali  waranti ya  kukamatwa kwa gavana wa machakos Alfred Mutua  ikisema inakiuka haki zake za kikatiba . korti pia imemzuia  inspekta mkuu wa polisi  dhidi ya kuchukua hatua kuhusiana na waranti hiyo  hadi kesi hiyo  isikizwe na kuamuliwa .

Rais Uhuru   Kenyatta amepongeza makundi ya uokoaji wa dharura yaliyoko katika Uwanja wa Ndege wa Wilson, Jijini Nairobi, kwa kuchukua hatua za haraka kufuatia ajali iliyohusisha ndege ya shirika la Silverstone aina ya Fokker 50.Wakati huo huo, Rais amewatakia uponyaji wa haraka waliojeruhiwa katika ajali hiyo ya ndege.

Iwapo kuna binadamu anayeweza kuvunja rekodi ya saa mbili ya mbio za marathon ,basi ni Eliud Kipchoge . Hii ndio kauli ya waziri wa michezi Amina Mohamed  ambaye anampigia upatu Kipchoge  kuivunja rekodi  hiyo  hapo kesho  endapo kila hali  itakuwa nzuri .

Chuo kikuu cha Moi kimefungwa kwa muda usiojulikana baada ya  wanafunzi kuzua rabsha  wakilalamikia  usimamizi mbaya . wanafunzi wamehamakishwa na kuongezwa kwa ada ya mtihani  wa ziada na kanuni mpya kuhusu  matumizi ya vyumba wanavyotumia kulala . ada ya mtihani wa ziada imezidishwa hadi shilingi 1000 kutoka shilingi 400.

Sarah Wairimu,  ,mjane wa raia wa udachi  marehemu Tob Cohen  ameachiliwa huru kwa dhamana  . sarah ambaye ndiye mshukiwa mkuu katika mauaji ya mumewe ameachiliwa na mahakama kwa dhamana ya shilingi  milioni 2 pesa taslimu .hata hivyo jaji Stella Mutuku ameamuru kwamba sarah hafai kukaribia majengo ya biashara za marehemu Cohen .

Kaunti ya taita taveta imeanza kuwahesabu  wafanyikazi wake  katika jitihada za kuwaondoa wafanyikazi feki na kuboresha utoaji wa huduma kwa wananchi . mkurugenzi wa mawasiliano wa kaunti hiyo  Dennis Onsarigo  amesema wakati wa shughuli hiyo ya siku mbili wafanyikazi wote watahitajika kuripoti katika  afisi za kaunti ndogo na  yeti vyao vya masomo pamoja na barua za uteuzi .

Huku hayo yakiarifiwa  Notisi ya kuondolewa afisini  kwa gavana wa kaunti ya Taita Taveta Granton Samboja sasa imewasilishwa kwa spika wa seneti Ken Lusaka.Waakilishi  wa wadi waliwasilisha notisi hiyo mapema hii leo huku Lusaka sasa akitarajiwa kuanza mchakato wa kuchunguza madai yaliyoibuliwa katika hoja ya kumbandua Samboja Katika kipindi cha siku saba kwa mujibu ya sheria Kama  anavyoeleza mwenyekiti wa kamati ya bajeti GODWIN KILELE.

Bunge la  Kaunti ya Trans Nzoia  leo  limewaalika wananchi kutoa maoni yao kuhusu mswada wa punguza mizigo .matokeo ya  mchango huo wa wananchi  yataamua iwapo  waakilishi wa kaunti hiyo wataupitisha au kuukata mswada huo uliopendekezwa na muungano wa Thirdway Alliance .

Oparesheni ya kuiondoa miili ya mama na mwanawe waliotumbukia katika bahari hindi huko likoni inaendelea huku serikali ikiwa na matumaini ya kumaliza  shughuli hiyo hivi leo . msemaji wa serikali Cyrus Oguna  amewarai wakenya kuwa na subira  kwani wanafnya kila wawezalo kuiondoa miili hiyo ,baada ya siku 13 .

Huku ulimwengu ukiadhimisha siku ya  mtoto wa kike leo ,wahadhiri wa kike kutoka chuo kikuu cha kibabii wametoa msaada wa vitambaa vya hedhi ya wasichana wa shule huko bungoma .wakiongozwa na  Caroline Namunan ,WAHADHIRI  hao wamesema  wasichana wa shule hasa katika maeneo ya mashambani hupitia changamoto kubwa kwa ajili ya ukosefi wa vitambaa hivyo na baadhi yao hukosa kwenda shule wakati wanapopata hedhi .

Waziri mkuu wa Ethiopia  Abiy Ahmed  ameshinda tuzo ya mwaka huu ya amani ya Nobel . kamati  ya tuzo hiyo kutoka Norway imetoa tangazo hilo la kumpa Abiy  taadhima hiyo kwa ajili ya juhudi zake za kuleta amani kati ya Ethiopia na taifa jirani la Eritrea  kwa ajili ya mzozo wa muda mrefu wa mpakani . Ahmed alitajwa kuwa mshindi wa 100 wa Nobel Peace Prize huko Oslo.