Afisa wa polisi kushtakiwa kwa kuvunja bavu ya makanga

Afisa wa polisi ambaye alimvamia na kuvunja bavu ya makanga katika kituo cha basi ya Kwavonza kaunti ya Kitui anatarajiwa kufikishwa mahakamani na kufunguliwa mashtaka.

Inadaiwa afisa huyo alikuwa amelewa kupindukia jambo ambalo ilichangia yeye kufanya tendo hilo.

Alfred Mutua ambaye ni muathirika wa tukio hilo anataka haki ifanyike manake afisa huyu alimpiga na kumjeruhi bila uchochezi wowote na hivyo basi hawezi fanya kazi kwani hana budi kutulia kwa nyumba hadi majeraha yake yapone.

Mutua ambaye alisema alipigwa hadi akapoteza fahamu alisaidiwa na dereva wa teksi ambaye alimpeleka hospitalini kupata matibabu ya dharura.