Afisa huyo alikamatwa pamoja na wado wake wanne Jane Chepkemei (CP No. 83816), Bernard Macharia ( PC No.110581), Samuel Maina ( PC No.119196) na Rodrick Laushuset (PC No. 59664).
Ripoti ya polisi inaonyesha kwamba walikamatwa baada ya kuiba pombe ya White Pearl Vodka kutoka kwa lori ambalo lilipata ajali wakati lilipokuwa likisafirisha pombe hiyo . Ajali hiyo iliyohusisha lori la Isuzu KCK 959L haikusababisha majeraha ya waliokuwemo .
Polisi hao wanadaiwa kuiba pombe hiyo badala ya kuilinda na baadaye chupa 72 za kileo hicho zilipatikana katika nyumba ya OCS Cheruiyot .
Tukio hilo liliripotiwa katika kituo cha polisi cha Ahero ,kaunti ndogo ya Nyando kupitia nambari ya OB OB3/10/08/2020 NA 41/10/2020.
OCS huyo alizuiliwa katika kituo cha polisi cha Kisumu Central .