Aibu gani? OCS Miongoni mwa waliokamatwa kwa kuiba pombe Kisumu

pjimage (7)
pjimage (7)
OCS  wa kituo cha polisi cha Boya huko Kisumu  chief inspector William Cheruiyot  ni miongoni mwa maafisa wa polisi waliokamatwa siku ya jumatatu kwa kuiba pombe .

Afisa huyo alikamatwa  pamoja na wado wake wanne  Jane Chepkemei (CP No. 83816), Bernard Macharia ( PC No.110581), Samuel Maina ( PC No.119196)  na  Rodrick Laushuset (PC No. 59664).

Ripoti ya polisi inaonyesha kwamba  walikamatwa baada ya kuiba pombe  ya White  Pearl  Vodka kutoka kwa lori ambalo lilipata ajali wakati lilipokuwa likisafirisha pombe hiyo . Ajali hiyo iliyohusisha lori la Isuzu  KCK 959L  haikusababisha majeraha ya waliokuwemo .

Polisi hao wanadaiwa kuiba pombe hiyo badala ya kuilinda  na baadaye chupa 72 za kileo hicho zilipatikana katika nyumba ya OCS Cheruiyot .

Tukio hilo liliripotiwa katika kituo cha polisi cha Ahero  ,kaunti ndogo ya Nyando  kupitia   nambari ya OB  OB3/10/08/2020  NA  41/10/2020.

OCS  huyo alizuiliwa katika kituo cha polisi cha  Kisumu Central .