Alidhani albamu yetu haitafana! Ethics na Octopizzo wajibizana

Ethic--1024x681
Ethic--1024x681
Majibizano baina ya wanamuziki wa kikundi cha Ethics na msanii wa hip hop nchini Otopizzo yanazidi kuibua hisia mseto baada ya Ethics kudai kuwa Octopizzo alikataa kushirikishwa katika albamu yao akidhani haitafanya vyema .

Kupitia mtandao wao wa twitter, Ethics waliandika kuwa Khaligraph Jones anafanya vyema kuliko Octopizzo, semi ambazo zilimpelekea Octo kujibu kuwa ni kutokana na hatua yake ya kukataa kushirikishwa katika albamu ya wasanii hao.

“Aaah is it because I refused to jump on your project or? Anyway, it is life. Wakiritho TA!TA!” Octopizzo alisema

Ethics walilazimika kujibu madai hayo kati yao.

“We gave @OCTOPIZZO the privilege to be on our super dope album but hakuona vision, truth ni numbers ziko but ange kuja tu na zile mathogothanio zake, video for the song wasn’t part of the plan…all in all watch out June 13th album dropping, ‘BIG MAN BADO ODINARE’ Ni mbwaya ni moto” Ethic waliandika

Ethics aidha siku za hivi maajuzi wamekuwa wakikashifiwa na wakenya kutokana na nyimbo zao kuwa za uzushi haswa zinazozungumzia maswala kuhusiana na ngono kila mara..