Alikiba, kama uzee unakuzuia kutoa ngoma tufahamishe

kiba.jfif
kiba.jfif

NA NICKSON TOSI

Msanii wa bongo raia wa Tanzania Ali Kiba amejitokeza na kukiri kuwa hajakuwa akitoa mziki kwa muda japo yumo jikoni kupika kibao ambacho anaamini kitatamba.

Katika kikao na wanahabari, Kiba alisema kwamba anapenda kufanya mziki ambao akiutoa utakubalika na wengi na kwa muda mrefu.

'Mimi sidhani kama eti nimeshuka ama nimekuwa mzembe kwa kazi yangu. Mziki ndivyo ulivyo kila biashara ina wakati wake na nilikaa miaka mitatu kabla,  Lakini nimerelease nyimbo mwaka jana inaitwa Mshumaa.. Mashabiki wanataka kila siku na inastahili wapewe. Mimi nataka wanisamehe na waelewe lengo la mziki wangu na thamani ya mziki ambao naufanya. Ninafurahi Zaidi nikitoa ngoma ambayo inakufurahisha. Nachukua muda wangu. Lakini vile vile wasanii wangu ilikuwa bado hawajatoa nyimbo so imepelekea mimi kupumzika kidogo na kuconcerntrate na wao mpaka wamalize kufanya video na nyimbo zao zitoke zote. Sasa hivi amebaki msanii mmoja ambaye nataka. ' alisema Alikiba.

Baba huyo wa watoto watano alisema hayo wakati wa uzinduzi wa Samakiba ambayo ni mashindano ya michezo ya kandanda chini ya udhamini wake.

Samakiba ni mashindano yalioanzishwa na Alikiba kwa ushirikiano na mshambulizi wa timu ya Aston Villa Mbwana Samatta, lengo kuu likiwa ni kuimarisha na kukuza talanta katika mitaa ya mji wa Dar es Salaam ,Tanzania.