AMEFAULU!! Eliud Kipchoge amaliza mbio chini ya masaa mawili

Amini usimamini! Mkenya na bingwa wa mbio za nyika kote duniani, Eliud Kipchoge amefaulu katika juhudi zake za kukamilisha mbio za Ineos1:59 challenge chini ya masaa mawili.

Kipchoge amemaliza mbio hizo baada ya lisa moja, dakika 59 na sekunde 40 pekee. 1:59:40.

Siku hii ndiyo iliyokuwa imengojewa dunia nzima huku kila mmoja akitazamia Eliud Kipchoge kuivunja rekodi yake na kumaliza mbio za kilomita 42, chini ya masaa mawili.

Mbio hizo maalum zijulikanazo kama Ineos1:59 challenge zilifanyika Vienna, Austria kuanzia mida ya 9:15  Jumamosi asubuhi na Kipchoge alisindikizwa na zaidi ya waweka kasi 20.

Hongera Kipchoge!!!