ANGEL OR DEVIL : Jinsi mwanamke ‘Tajiri zaidi Afrika’ Isabel dos Santos alivyoipora Angola.

Stakabadhi zimetolewa  na kufichua jinsi  Isabel Dos santos ,bintiye  rais wa zamani wa  Angola Eduardo dos santos alivyopora mali ya umma nchini humo ili kujimbikikizia kiasi kikubwa cha mali .Isabel dos Santos  alipata kandarasi kubwa kubwa za mabilioni ya dola  katika  mikataba ya mashamba ,madini  ,mafuta na sekta ya mawasiliano wakati babake alipokuwa uongozini .Ufichuzi ulotolewa sasa umebaini kwamba yeye na mume wake waliruhusiwa kununua mali za serikali zenye thamani kubwa katika  mauzo yanayozua shauku . Bi Dos santos amedai kwamba madai dhidi yake ni ya hila na kwamba yamechochewa kisiasa  . Tangu babake aondoke maamlakani ,familia ya Dos Santos imekuwa ikilalamika kwamba inalengwa na serikali ya  rais mpya  João Lourenço.  Binti huyo wa rais wa zamani amehamia  Uingereza na anamiliki mali nyingi katikati mwa jiji la London . Tayari maamlaka nchini Angola zinamchunguza kwa wizi wa mali ya umma na baadhi ya mali yake imebanwa na kuwekwa chini ya usimamizi wa serikali .

Uchunguzi uliofanywa na mashirika mbali mbali ya vyombo vya habari na kueteta haki za binadamu umeonyesha kwamba  nyingi ya mali inayomilikiwa na Bi Dos santos  ilipatikana kwa njia isio halali na iliyozidi kuwafilisi wananchi wa Angola . Kuna pengo kubwa zaidi kati ya watu maskini na matajiri nchini humo na mafanikio yaliyoletwa na uchimbaji mafuta na pato la madini haujaweza kuwatiririkia raia wa kawaida nchini humo.

Hilo limelaumiwa kusababishwa na  ubinafsi na ulafi wa watu wenye  maamlaka na uwezo wa kupora mali ya umma bila kuogopa  matokeo yoyote kama vile Bi Isabel. Mojawapo ya wizi mkubwa sana uliotekelezwa nchini Angola ni kupitia kwa kampuni moja iliyosimamiwa kutoka London yenye uhusiano na kampuni ya  mafuta ya  Angola  Sonangol.Bi Isabel alipewa jukumu la kuisimamia kampuni hiyo mwaka wa 2016  kwa sababu ya agizo la rais , babake  Jose Eduardo Dos Santos  ambaye aliiongoza nchi hiyo kama mali yake kwa miaka 38 . Lakini babake alipostaafu mwaka wa 2017 ,nafasi ya Isabel katika kampuni ya Sonangol ilikuwa hatarini na muda mfupi baadaye  alifurushwa kutoka nafasi hiyo na rais mpya  Joao Lourenço ambaye pia ameamua kuitwaa mali ya baadhi ya watu wa familia ya  mtangulizi wake . Raia wengi wa Angola   wameshangazwa  kutokana na jinsi rais Joao Lourenço  anavyokabiliana na  uha,lifu uliiotekelezwa na watu wa familia ya mtangulizi wake .