Baraza la magavana limeonya kuhusu kuvunjwa kwa bunge kufuatia ushauri wa jaji mkuu David Maraga kwa rais Uhuru Kenyatta .
Kupitia taarifa siku ya jumatano mwenyekiti wa COG Wycliffe oparanya amesema ingawaje wanaelewa msimamo wa jaji mkuu kuhusu suala hilo ,kwa sasa kutakuwa na athari kubwa kwa taratibu za serikali endapo bunge litavunjwa hasa wakati huu ambapo serikali inapambana na janga la corona .
" Kwa sasa taifa lipo katika mjadala wa uwezekano wa kuirekebisha taifa …huu sasa ndio wakati wa kuyazingatia mapendekezo yote kuhusu usawa wa kijinsia na kuhakikisha kwamba kanuni hiyo inatekelezwa k iwapo marekebisho ya sharia yataafikiwa’ amesema Oparanya
Maraga siku ya jumatatu alimshauri rais Uhuru Kenyatta kulivunja bunge kwa kukosa kutekeleza kanuni ya usawa wa kijinsia