Yaonekana Dennis Itumbi amependwa na wengi lakini pia ana wengia mabo hawana huruma naye . Baada ya kufutwa kazi katika wiki ambayo ilikuwa pia birthday yake Itumbi huenda akajipata na masimango si haba mtandaoni .
Kwa mfano Profesa Makau Mutua ametumia Twitter kuonyesha furaha yake kuhusu yaliomsibu Itumbi .Amesema ingawaje sio kawaida yake kufurahia matatizo ya wengine , hatojibana ili kupiga tosti glasi ya kinywaji baada ya Itumbi kuonyeshwa mlango wa Ikulu.Tazama ujumbe alioandika katika twitter
https://twitter.com/makaumutua/status/1240393757763256321
Itumbi alikuwa mkurugenzi mkuu aliyesimamia mawasiliano ya kidijitali . Nafasi nyingine zilizofutiliwa mbali ni mkurugenzi mkuu wa mawasiliano anayesimamia hafla , mkurugenzi mkuu anayesimamia uandhishi wa hotuba na afisa mkuu wa mawasiliano . Nafasi hizo nyingine zilikuwa zikishikiliwa na James Kinyua, Erick Ng’eno, David na John Ndolo. Katika maelezo kumhusu katika twitter ,Itumbi amejieleza kama mfungaji wa nguruwe . Kupoteza kazi yake kumejiri wiki hii ambayo alishehekea siku yake ya kuzaliwa . Itumbi amekuwa katikati ya kesi inayohusisha barua iliyokuwa na madai ya njama ya kumuua naibu wa rais William Ruto .