Klabu ya daraja la pili Derby County imemtaja mfungaji bora wa Uingereza, Wayne Rooney kama kocha mkuu kwa mkataba wa miaka miwili na nusu.
Rooney mwenye umri wa miaka 35 amekua akihudumu kama kocha wa muda baada ya kocha mkuu Phillip Cocu kuchujwa Novemba tarehe 14. Rooney sasa amestaafu rasmi kutoka soka, na atapambana kuwaepusha vijana wake na shoka kwani wanashikilia nafasi ya 22 kwenye jedwali.
Kiungo wa Manchester United Bruno Fernandes jana alitajwa kama mchezaji bora wa ligii ya EPL wa mwezi Disemba. Fernandez sasa ameshinda taji hilo mara nne msimu huu na kufikia rekodi ya wachezaji wa zamani Paul Scholes na Cristiano Ronaldo ugani Old Trafford . Fernandez amesalia na taji moja la mcheaji bora wa mwezi nchini Uingereza ili kufuikia rekodi ya washambulizi wa zamani Wayne Rooney na Robin van Persie.
Mshambulizi wa Ulinzi stars Enosh Ochieng atakosa mechi za ligi kuu nchini kwa miezi mitatu, baada ya kuondoka kufanya masomo zaidi ya kijeshi. Ochieng ambaye ni mwan jeshi alinyakua taji la mfungaji bora katika ligi mwaka wa 2018, na kocha mkuu Dunstan Nyaudo anadai watazikosa sana huduma zake. Ochieng ni mmoja wa wachezaji ambao wanakwenda kwa masomo zaidi kama ilivyo desturi ya kikosi hicho cha Nakuru.