KOT wakemewa kwa kumshambulia Kanze Dena

Achaneni na Kanze Dena! Mastaa wa kike wajitokeza kuwakemea KOT

Mtangazaji wa radio Jambo Massawe Japani pia aliadika ujumbe kulaani waliokuwa wakimfanyia masihara na kumtupia vijembe Kanze kwa ajili ya muonekano wake

Muhtasari
  • Wa hivi pundi kujipata katika upande wa  kupondwa na KOT ni msemaji wa Ikulu Kanze Dena ambaye wengi walitumia mitandao ya kijamii kueleza kushangazwa kwao  kutokana na kuongeza uzani .
  •  Nyota wa muziki Wahu ni miongoni mwa walioonekana kukerwa na tabia hiyo ya KOT na akaeleza msimamo wake .

 

Kanze Dena

 Watumiaji wa mitandao wanaweza  kuwa na ukatili na wakati mwingine ukatili huo huvuka mipaka . Wa hivi pundi kujipata katika upande wa  kupondwa na KOT ni msemaji wa Ikulu Kanze Dena ambaye wengi walitumia mitandao ya kijamii kueleza kushangazwa kwao  kutokana na kuongeza uzani .

Kanze Dena

Hata hivyo mastaa mbali mbali haa wa kike  nchini wamejitokeza kulaani vitendo vya baadhi ya watumiaji wa mitandao kumfedhehsha mtu kwa maneno makali na ukatili kwa ajili ya kuongeza kilo n na hasa mtu ambaye amepata mtoto  hivi karibuini

 Nyota wa muziki Wahu ni miongoni mwa walioonekana kukerwa na tabia hiyo ya KOT na akaeleza msimamo wake .

 Mtangazaji wa radio Jambo Massawe Japani pia aliadika ujumbe kulaani waliokuwa wakimfanyia masihara na kumtupia vijembe Kanze kwa ajili ya muonekano wake

 Msemaji huyo wa Ikulu na mkuu wa PSCU  alikuwa akizungumza  katika Ikulu  ndogo ya Sagana  siku ya ijumaa  wakati rais Uhuru Kenyatta alipokuwa akijitayarisha kuanza ziara  ya siku nne katika eneo la kati