- Wa hivi pundi kujipata katika upande wa kupondwa na KOT ni msemaji wa Ikulu Kanze Dena ambaye wengi walitumia mitandao ya kijamii kueleza kushangazwa kwao kutokana na kuongeza uzani .
- Nyota wa muziki Wahu ni miongoni mwa walioonekana kukerwa na tabia hiyo ya KOT na akaeleza msimamo wake .
Watumiaji wa mitandao wanaweza kuwa na ukatili na wakati mwingine ukatili huo huvuka mipaka . Wa hivi pundi kujipata katika upande wa kupondwa na KOT ni msemaji wa Ikulu Kanze Dena ambaye wengi walitumia mitandao ya kijamii kueleza kushangazwa kwao kutokana na kuongeza uzani .
Hata hivyo mastaa mbali mbali haa wa kike nchini wamejitokeza kulaani vitendo vya baadhi ya watumiaji wa mitandao kumfedhehsha mtu kwa maneno makali na ukatili kwa ajili ya kuongeza kilo n na hasa mtu ambaye amepata mtoto hivi karibuini
Nyota wa muziki Wahu ni miongoni mwa walioonekana kukerwa na tabia hiyo ya KOT na akaeleza msimamo wake .
Mtangazaji wa radio Jambo Massawe Japani pia aliadika ujumbe kulaani waliokuwa wakimfanyia masihara na kumtupia vijembe Kanze kwa ajili ya muonekano wake
Msemaji huyo wa Ikulu na mkuu wa PSCU alikuwa akizungumza katika Ikulu ndogo ya Sagana siku ya ijumaa wakati rais Uhuru Kenyatta alipokuwa akijitayarisha kuanza ziara ya siku nne katika eneo la kati