Sikuua mtu kwa kuwa mke wa pili wa Jimal-Amber Ray amwambia mke mwenza Amira

Muhtasari
  • Amber Ray asema hakuua mtu kwa kuwa mke wa pili
  • Amber alisema kuwa yeye ni mke wa pili tu na hajaua mtu yeyote kustahili chuki zote

Mwanasosholaiti  Faith Makau maarufu Amber Ray, amepakia video kwenye youtube, akisimulia upande wake wa hadithi drama yake na mke mwenza wake Amira iliyotokea jumanne.

Amber alisema kuwa yeye ni mke wa pili tu na hajaua mtu yeyote kustahili chuki zote zinazoelekezwa kwake.

"Hata ikiwa mimi ni mke wa pili sijaua mtu yeyote na nimekuwa nikipata chuki nyingi na nguvu hasi kutoka kwa mitandao ya kijamii na yote ni kwa sababu ya hii. Nilifikia hatua ilibidi nisimame mwenyewe.

Huwezi kuendelea kunitukana kutumia maisha yangu ya zamani kunifanya nionekane mbaya. Katiba imekubali, hata ikiwa mimi ni mke wa pili, sijaua mtu yeyote… unajaribu sana kunivuruga. hata hiyo siku angekuja tu na kubisha mahali pangu sio mtu mwenye wazimu ati nimvuruge… Sijali kusikiliza hadithi yake lakini usinisulubishe kwa sababu mimi ni mke wa pili.

Kama jamii najua ni ngumu kuwa mke wa pili lakini hii ndio inafanyika leo. Kwa kiasi kikubwa kama unakataa kushare, tunashiriki ”Amber Ray alielezea.

Sosholaiti huyo alimshtaki Amira kwa kuwa mtu wa kujifanya ambaye kila wakati anatafuta huruma kwenye mitandao ya kijamii kwa kujifanya ndiye asiye na hatia.

Usijaribu kuja katika maisha yangu na kuamuru jinsi ninapaswa kuishi maisha yangu. Acha kila mtu aishi maisha yake. Ua Mtu aaangalie Kwake. Na ikiwa heshima yake ni lazima ijiheshimu wewe mwenyewe, kwa mimi kukuheshimu wewe ... mimi ni mwanadamu na mimi ni wa mitaa nitapambana. Niko hapa ili kukanyagwa.

Ilikuwa chaguo la Jamal kunifanya kuwa mke wake wa pili na sikuua mtu yeyote "alisema Amber Ray kwa sehemu