Siwezi msamehe mwanamume anaetelekeza mwanamke akiwa mjamzito-Jovial

Muhtasari
  • Kulingana na mwanamke huyo alipata ujauzito na aliyekuwa mpenzzi wake na kisha akamtoroka, baada ya miaka 5 amerudi na anataka warudiane
Jovial in red
Jovial in red

Jovial ni msanii ambaye amefahamika sana kutoka na kazi yake ya usanii, Msanii wa kike wa  amejitokeza wazi kutangaza maoni yake na kusema hawezi kumsamehe mwanamume anayemtelekeza mwanamke ambaye ni mjamzito.

Jovial alikuwa anatoa maoni yake kuhusu chapisho ambalo lilichapishwa mitandaoni huku mwanamke akisimulia jinsi baba ya mtoto wake alimuacha baada ya kupata ujauzito wake.

Kulingana na mwanamke huyo alipata ujauzito na aliyekuwa mpenzzi wake na kisha akamtoroka, baada ya miaka 5 amerudi na anataka warudiane.

Huku msanii huyo akimpa mwanamke huyo ushauri alimwambia kwamba;

"Siwezi msamehe mwanamume anaetelekeza mwanamke akiwa mjamzito,mimba ni kama ugonjwa Mungu wangu asikwambie mtu

Unahitaji upendo wote, mshukuru MUngu kama safari yako ilikuwa rahisi, miaka 5 mbaadaye heri angekuwa nakujulia hali mara kwa mara, kwa nnini ajitokeze sasa hivi namuimba MUngu usimpoteze mwanamume mzuri," Joviala alimshauri mwanamke huyo.