Nakupenda sana usinisahau,'Ali Kiba amwambia mwanawe

Muhtasari
  • Ijumaa wiki hii msanii huyo aligonga vichwa vya habari baada ya mkewe kutaka talaka
  • Wanamitandao walishangazwa kwani wawili hao walionekana kupenda na ndooa yao kutamanika na wengi

Halizuki jambo bila mwenyezi Mungu kutaka yote, haya ni matamshi ya staa wa bongo Alikiba, huku akimtakia mwanawe siku njema ya kuzaliwa.

Ijumaa wiki hii msanii huyo aligonga vichwa vya habari baada ya mkewe kutaka talaka.

Wanamitandao walishangazwa kwani wawili hao walionekana kupenda na ndooa yao kutamanika na wengi.

Leo Jumamosi ikiwa ni siku maalum ya mwanawe Alikiba kupitia kwenye ukurasa wake wa instagram alimwambia mwanawe kwamba anampenda na kwamba kwa lolote asimsahau.

"Halizuki jambo bila Mwenyezi MUNGU kutaka yote KheriHappy birthday SON NAKUPENDA SANA Usinisahau ❤️,"Alikiba Ameandika.

NI ujumbe ambao uliibua hisia tofauti kutoka kwa mashabiki wake, na hizi hapa baadhi ya hisia zao;

tumusiime_1: You've been through alot till this stage of your life and career! This too will pass bro! Take heart!

vj_cholo: Toa talakaa wakenya nao watu mkome kuoa nchi mbali toa talaka tuwaite azam kama mlivyo tukeshesha kutazama harusi yenu ndio tutakesha kuachana kwa kiba ba amina

official_tachtzIla:  Mimi nakushauri kaka ustoee talaka kabsaaaaa 😂😂

itsray340: Mjifunze kuithamini familia kwanza kabla ya wengine.hbd mtoto mzuri.

barbie_mg54: Hata alieimba wimbo wa utu na yeye pia chaka lake limefyekwa kweli uchawai upo😢