Diamond na Zari wasifiwa wanapendeza pamoja, waombwa warudiane

Baadhi walionekana kutomkubali kabisa mpenzi wa sasa wa Diamond, Zuchu.

Muhtasari

•Wanamitandao wengi wakipendekeza  kuwa wawili hao waonekana wazuri pamoja kama wanandoa. Baadhi waliwaomba warudiane.

•Baadhi waliibua tetesi kuwa mwanasoshalaiti huyo alitumia akaunti ya Tiffah kujieleza jinsi anavyomkosa Diamond  maishani.

Diamond Platnumz, Prince Nillan, Tiffah Dangote na Zari Hassan
Image: INSTAGRAM// ZARI HASSAN

Siku ya Ijumaa, picha ya Diamond, Zari na watoto wao wawili ilichapishwa kwenye ukurasa wa Instagram wa Tiffah Dangote.

Tiffah ni mtoto wao wapenzi hao wa zamani wa kwanza ambaye ana umri wa miaka 6. Wawili hao pia wana mtoto mwingine wa kiume anayefahamika  kama Prince Nillan ambaye ana umri wa miaka mitano.

"Pamoja na wazazi wangu," yalisomeka maandishi  yaliyowekwa chini ya picha hiyo nzuri ya kumbukumbu ambayo iliwaonyesha Diamond na Zari wakiwafundisha watoto hao wao kuendesha baiskeli.

Picha na ujumbe huo ziliwasisimua watumizi wengi wa Instagram wengi ambao walifurika pale kutoa maoni yao.

Chini ya chapisho hilo, jumbe  nyingi za sifa kwa wazazi hao wenza zilimiminika huku wengi wakipendekeza  kuwa wawili hao waonekana wazuri pamoja kama wanandoa. Baadhi waliwaomba warudiane.

Katika sehemu ya maoni, baadhi ya wanamitandao walionekana kutomkubali kabisa mpenzi wa sasa wa Diamond, Zuchu na kumshauri kuwa mzazi mwenzake Zari Hassan anatengeneza mpenzi bora kwake.

"Sana tuache unafiki Mondi (Diamond)  akiwa na Zari hadi familia inakuwa kama ya heshima lakini akiwa na hivi vikwakwa mtumeee wanaonekana kama wamechanganyikiwa ," @vaneismail alisema.

@jira_laporte alisema, "Diamond akiwa na Zari ywavaa smart as a gentle Man... lakini akiwa na vile vikenge vyavaa kama chizi flani ivi....We Mond baki uko kwa zari anakufanya uonekane mtu mzima na mzuri wa juu."

@mkendenzua alisema, " Fanyeni kama mrudiane hivi tunawamiss sana mashabiki."

@fridanicols, " Wakweli. Huko kwingine shauri yake bana. Wanapendeza  hata kufuatilia mienendo zao."

"Tuendelee ila ipo siku Tiffah atarudisha hii familia pamoja," alisema @legit_queen_z.

Zari ndiye anasimamia akaunti za Tiffan na Nillan. Baadhi ya wanamitandao waliibua tetesi kuwa mwanasoshalaiti huyo alitumia akaunti ya Tiffah kujieleza jinsi anavyomkosa Diamond Platnumz  maishani.

Diamond alijibu chapisho hilo kwa emoji ya upendo "❤"

Haya yanajiri siku chache tu baada ya mzaliwa huyo wa Uganda kutangaza  atakuwa nchini Tanzania katika kipindi cha  Krismasi.

Zari alishiriki mazungumzo ya simu na Mama Dangote ambapo alimthibitishia kuhusu ziara hiyo. Alimwambia mzazi huyo wa Diamond kwamba atawapeleka wajukuu wake Tiffah Dangote na Prince Nillan ili waweze kufurahia muda na wanafamilia wengine.

Katika mazungumzo hayo, Zari ambaye kwa sasa anaishi na familia yake Afrika Kusini alidokeza kuwa mpango wa kusherehekea sikukuu ya Krismasi nchini Tanzania ni uamuzi ambao alifanya pamoja na Diamond.

"Baba yao amesema wanakuja Krismasi. Bado tuko shule," Zari alimwambia Mama Dangote katika mazungumzo.

Hii haitakuwa mara ya kwanza kwa Zari Hassan na watoto wake kutembelea familia ya kina Diamond katika miaka ya hivi majuzi. Mfanyibiashara huyo mwenye umri wa miaka 42 bado huwa anatembea nyumbani kwa mzazi huyo mwenzake licha ya wao kutengana takriban miaka minne iliyopita.