YouTube yatoa orodha ya miamba wa Afrika 2021

Muhtasari

• Usimamizi wa Youtube umetoa orodha ya wasanii kumii wa eneo la jangwa ya kusini waliofanikiwa kuwa na watazamaji wengi katika mtandao huo katika mwaka wa 2021.

• Orodha hii ambayo imewajumuisha wasanii wawili kutoka taifa la Tanzania, huku asilimia kubwa ikiwa wasanii wa Nigeria.

Usimamizi wa Youtube umetoa orodha ya wasanii kumii wa eneo la jangwa ya kusini waliofanikiwa kuwa na watazamaji wengi katika mtandao huo katika mwaka wa 2021.

Orodha hii ambayo imewajumuisha wasanii wawili kutoka taifa la Tanzania, imeibua maswali mengi miongoni mwa mashabiki huku wasanii wengi kwenye majina hayo wakionekana kutoka katika taifa la Nigeria.

sammisago
sammisago
Image: instagram KWA HISANI

Shughuli kama hizi mara si moja zimeonekana kuleta ugomvi baina ya wasanii, ya hivi karibuni ikiwa ile ya Forbes [kuhusu wasanii tajiri zaidi Afrika] ambapo msanii Diamond Platinumz alilazimika kuwajibu na kuwaambia kwamba kabla ya wao kuachia orodha hizo wawe wanafanya uchunguzi wao wa kina na kujua thamani yake ndani na nje ya muziki.

Mwaka huu wa 2022 wasanii wengi wameonekana kuachia kazi za kuburudisha huku wengi wakisubiria kuona nani atakuwa anaibuka kidedea mwishoni mwa mwaka huu kwa kuwa na watazamaji wengi zaidi katika mtandao wa YouTube.