Milly Wajesus na Kabi Wajesus wafichua jinsia ya mtoto wao wa pili

Muhtasari
  • Milly Wajesus na Kabi Wajesus wafichua jinsia ya mtoto wao wa pili
Image: INSTAGRAM// KABI WAJESUS

Waunda maudhui Kabi Wajesus na Milly Wajesu kupitia kwenye chaneli yao ya youtube siku ya Jumatano wamefichua jinsia ya mtoto wao wa pili.

Kulingana na wanandoa hao wawili wanatarajia mtoto msichana

Wakati wa uchunguzi huo, Kabi alisema atasikitika ikiwa atagundua kuwa alikuwa anatarajia mtoto mwingine wa kiume.

"Wakati huu mimi niko kwenye timu ya wasichana. Ikiwa ni mvulana, nitakatishwa tamaa. Ndivyo ilivyo. Nataka kuwa wazi kwa uhakika iwapo nitakatishwa tamaa na kuhisi nimeikubali," Kabi alisema.

Alieleza kuwa sababu ya yeye kutaka msichana ni kwamba mwanawe ameelekeza mawazo yake kwa mama yake.

"Taji anampenda mama yake kuliko mimi. Ikitokea kuwa mvulana, atampenda mtoto lakini atanyonya mwaka mmoja tunaanza kutafuta mwingine. Nataka msichana anikumbatie."

Ikiwa ni msichana, Kabi alidokeza kwamba atakuwa mtoto wake wa mwisho.

"Penzi langu litalazimika kunishawishi kupata mwingine. Ninahisi kwa vile sikuwepo kwa ajili ya maisha ya binti yangu katika umri wake mdogo, nataka kupata uzoefu wa upendo wa kulea mtoto wa kike."

Wanandoa hao walisema walitaka kujua jinsia kwanza ndipo wafanye ufunuo wa jinsia kwa marafiki zao, tofauti na mzaliwa wao wa kwanza Taji ambapo walikaa kwa miezi kadhaa kabla ya kujua jinsia.