Davido amwaga mamilioni kununua mkufu wenye kichwa cha sura ya Yesu

Davido alikuwa akitumbuiza kwa ajili ya albamu yake ya Timeless ambayo mwezi kesho inamaliza mwaka mmoja tangu aiachie rasmi mwaka jana.

Muhtasari

β€’ Kikiwa na karati mbili za emerald na vidokezo hamsini kwenye waridi, kipande hiki cha ajabu kilipambwa kwa karibu karati arobaini za almasi za rangi ya mviringo.

Davido azungumzia kupata mapacha.
Davido azungumzia kupata mapacha.
Image: Instagram

Mwimbaji wa Nigeria Davido, ambaye jina lake halisi ni David Adeleke, ameonyesha jinsi ya kutamba na utajiri wake baada ya kuonesha mkufu wa kifahari ambao ni wa dhahabu unaoundwa na sura yenye mfanano na ile ya Yesu.

Msanii huyo aliuonesha mkufu huo adimu unaometameta wikendi iliyopita akiwa katika shoo yake ya ukumbi wa 02 nchini Uingereza, London.

Davido alikuwa akitumbuiza kwa ajili ya albamu yake ya Timeless ambayo mwezi kesho inamaliza mwaka mmoja tangu aiachie rasmi mwaka jana.

Chioma Adeleke, mkewe, alikuwa mmoja wa wale waliokuwa 02 Arena kumtazama akitumbuiza kwa furaha ya mashabiki wake. Video inayovuma ilionyesha wakati alipopokea cheni hiyo ghali kutoka kwa sonara.

Kikiwa na karati mbili za emerald na vidokezo hamsini kwenye waridi, kipande hiki cha ajabu kilipambwa kwa karibu karati arobaini za almasi za rangi ya mviringo.

Mtengeneza vito aliyeunda kazi hii ya kusisimua ya sanaa alishiriki picha na video ya kazi yake nzuri ya mikono. Bosi wa DMW ni mmoja wa wengi waliopata cheni yaa shingoni ya Yesu.

Hapo awali tuliripoti kwamba mwimbaji wa Nigeria aliyeshinda Tuzo ya Grammy Burna Boy alidaiwa kumzawadia rafiki yake wa karibu na mfanyakazi mwenzake Phyno kishaufu chake chenye mandhari ya Yesu mwishoni mwa mwaka jana.