Usikuje dm yangu na ofa ya mapenzi pekee, kitu pekee ninakosa ni pesa - Pritty Vishy

“Msije kwa dm yangu ikiwa mnataka kunipa mapenzi pekee. Mkiona hii kumetameta mnadhani ni makaratasi inanifanya nimetemete?” Vishy aliuliza.

Muhtasari

• Vishy akionekana kutopuuzilia mbali dhana ya kupendwa, alisema kwamba wanaume wote wanaomtaka kimapenzi sharti wamuendee pamoja na pesa pia.

Aliyekuwa mpenzi wa Stivo Simple Boy, Pritty Vishy
Aliyekuwa mpenzi wa Stivo Simple Boy, Pritty Vishy
Image: SAIDI ABDALLA

Pritty Vishy ametoa onyo kali kwa wanaume ambao wameingia kwenye DM yake kwa kishindo baada ya kuenea kwa mahojiano yake hivi majuzi kwenye Obinna Show.

Akionyesha kero yake kupitia instastory, Pritty Vishy alisema kwamba amechoka kusoma jumbe za wanaume wanaompa ahadi za mapenzi, akisema kwamba anachokihitaji kwa sasa si mapenzi bali ni pesa.

“Kwa wale wanaume wote wanaonipigia simu na kuniandikia jumbe kwa kuhisi kwamba ninakosa mapenzi kwa sababu ya babangu na kile nilichosema kwenye Obinna Show, ndugu zangu, niacheni peke yangu, kitu ninachokosa ni pesa,” Pritty Vishy alisema.

Vishy akionekana kutopuuzilia mbali dhana ya kupendwa, alisema kwamba wanaume wote wanaomtaka kimapenzi sharti wamuendee pamoja na pesa pia.

“Msije kwa dm yangu ikiwa mnataka kunipa mapenzi pekee. Kama unataka kunipa hayo mapenzi, hakikisha unanipa pia na hizo pesa. Mkiona hii kumetameta mnadhani ni makaratasi inanifanya nimetemete?” Vishy aliuliza.

Vishy pia alipata uwazi kuhusu jinsi anavyojiona akiangazia jinsi anavyojua kuwa hatamaniki au kuwa mrembo kutazamwa, jambo ambalo linaumiza sana kama inavyoonyeshwa na machozi yake ya kihisia.

"Mimi mimi ni mbaya! Kwanini yule jamaa amwache mpenzi wake na kuja kwangu? Nina nini cha kutoa? Mimi ni mbaya," alisema mwanamuziki huyo chipukizi kwa njia ya ukweli kwamba mtangazaji wa kipindi alibaki ameduwaa sana asiweze kuongea.

Baada ya kusema na kushughulikia yale aliyokuwa ametoka kuyasikia, Obinna aliendelea kumuuliza mgeni wake kama kweli alimaanisha kile alichokuwa ametoka kusema kuhusu yeye mwenyewe.