Covid-19: Msadieni huyu dada! Kisa cha kuhuzunisha cha msichana mwenye akili taahira aliyetelekezwa KMTC

Inapitia machungu  ya  kuhuzunisha familia moja kutoka Mombasa ambayo jamaa yao kutoka Dubai aliye na akili taahira anazuiliwa na serikali kwa siku 14 katika chuo cha KMTC huko Nakuru bila kumpa utunzi  na matibabu anayohitaji .

Irene  Nduta  mwenye umri wa miaka 50 ni mama mwenye huzuni na amelia hadi amekauka macho tangu   binti yake  Anne Wachuka  mwenye umri wa miaka 25 alipowasili nchini  Kutoka Dubai siku ya Jumatatu  na kutua katika uwanja wa JKIA .

“ Nilikuwa nimeenda kumpokea lakini nilipomuangalia, hakuwa sawa. Alionekana kuwa na mawazo’ Nduta amesema .

Nduta anasema kabla ya binti yake kuja Kenya akiwa  Dubai, alifahamu kwamba hali yake kiakili haikuwa nzuri kwani alipigiwa simu kuambiwa kuhusu  hali yake. Wafanyikazi  wenzake walikuwa wamesema kwamba  Wachuka alikuwa mgonjwa na alikuwa amelazwa hospitalini.Walimueleza kuwa binti yake hakuwa na nguo  na hakuna aliyekuwa akimtunza . Akikumbuka taswira hiyo ya mtoto wake, Nduta anabubujikwa machozi  kwani kando na hali ya mwanawe, pia ana ufahamu kwamba Wachuka na wakenya wengine waliokuwa wakifanya kazi ya usafi huko Dubai walikuwa wakiteswa na mwajiri wao .

Nduta alimpigia wakala aliyempeleka binti yake Dubai ili kujua kinachofanyika lakini akapuuza akisema binti yake alikuwa tu akifanya maigizo kwa sababu aliharibu vitu vya kampuni aliokuwa akiifanyia kazi . Baadaye Nduta  alipokea simu ya daktari mmoja kutoka Dubai aliyemuambia kwamba binti yake alikuwa mgonjwa na anahitaji msaada wa familia yake .

“ Daktari alipompa mtoto wangu simu Anne alisema  tu  ‘nakuja mama, nakuja mama’…  mananeno hayo yalinivunja moyo’ anasema. Nduta akibubujikwa machozi. Baadaye Nduta aligundua kwamba alihitaji sasa kumtumia  Wachuka nauli ya kurejea Kenya .

Nduta anasema  walipofika uwanja wa ndege wa JKIA , watu wote waliokuwa wakiwasili nchini walikuwa wakipelekwa katika taasisi za serikali kwa uangalizi kwa siku 14 kabla ya kuruhusiwa kwenda nyumbani. Anne alipelekwa katika chuo cha KMTC  Nakuru . “ Katik chuo cha KMTC  niliwarai polisi waniruhusu nimtunze lakini walikataa. Wasamaria wema walinipia simu wakiniambia kwamb Anne likuwa akilala nje ya jengo katika Corridor’ amesema. “ Mbona  serikali inamazui aondoke ili tumpe utunzi? Je, nitaweza kungoja kwa siku 14 kabla ya kumuona mtoto wangu? Serikali inafaa kunisaidia tafadhali ‘ anasema Nduta .

Nduta  ambaye sasa amelazimika kuishi  Nakuru na jamaa yake akingoja kuachiliwa kwa binti yake anasema amekuwa akiwatuma  binti yake mwingine na kakake yao kwenda kumuona Anne lakini hawaruhusiwi kuingia ndani .

" Siwezi kumtembelea kwa sababu ya umri wangu. Binti yake ameogopa kwa sababu iwapo walio ndani wana virusi vya Corona  basi nitaangamia’ anasema Nduta .