Visa vipya 104 vya coronavirus vimeripotiwa nchini katika saa 24 zilizopita baada ya sampuli 2,820 kupimwa.
Katibu wa utawala wa wizara ya Afya Rashid Aman amesema kwa jumla Kenya imefanya vipimo vya sampuli 136,361 hadi kufikia sasa
Kati ya visa hivyo vipya 76 ni vya wanaume ilhali 28 ni vya wanaume huku aliye na umri wa juu zaidi akiwa na miaka 76 .
Nairobi inazidi kuongoza kwa idadi ya juu ya visa hivyo baada ya 60 zaidi kuripotiwa kati ya 104 vya hivi leo Mombasa ina 33, Kilifi 5, Busia 3, Kajiado 2 na Taita Taveta 1.
Mjini , visa hivyo ni kama ifuatavyo katika mitaa : Langata 22, Kibra 19, Westland 11, Starehe 3, Dagoretti North 2, Embakasi South, Embakasi East na Kasarani kisa kimoja kila mtaa .
Idadi ya walioaga dunia kwa ajili ya virusi hivyo sasa ni watu 121 baada y watu 2 zaidi kuaga dunia . watu 36 wamepona ugonjwa huo na kufikisha jumla ya walipona kuwa 1586 .