“I went to do public health and the first assignment was in a morgue, which was not my thing. That pressure made me like the DJ part more.” Dj Nyc alisema.
Baada ya hayo ,Nyc alimpigia baba yake simu na kumwambia kuwa anataka kufanya kazi kwa radio na njia ambayo itamwezesha afanye kazi kwa radio ni kama atakuwa Dj.
Kwa mara ya kwanza, baba yake alikataa ombi lake lakini baada ya kusisitiza kuwa ile kazi ndio kazi ambayo anataka, baba yake alimlipia karo ya shule ya kusomea kuwa DJ baada ya kumhakikishia kuwa, atamaliza kozi yake ya afya ya jamii.
“At first he stopped me but I convinced him, and he paid my fees after I promised to finish my public health course,” Nyc alisema.
Nyc alikazana na kusoma kozi yake ya afya ya jamii na pia udj na baada ya miaka minne, alihitimu na kozi hiyo ya afya ya jamii. Hata hivyo, alisema na kusisitiza kuwa, hajawahi tumia digrii ile na mpaka wakati huu, mama yake humwona kama binti asiye na kazi.
“I have never used the degree anywhere and my mum still thinks I’m jobless.”
Safari ya udj, haijakuwa rahisi, kwani dj wengi wa kiume huwaona dj wa kike kuwa tishio kwao na kwa hivyo, wanakutishia na wengine kutaka kushirikiana na wewe kimapenzi ili wakupe kazi.
"It won’t be easy at the start, but focusing on what you want to achieve is the key.”Dj Nice alisema.