Msanii wa mkubwa Afrika Diamond Platnumz amefunguka muda mchache baada ya kupigiwa simu stejini na rais Pombe Magufuli.
Rais wa nchi jirani ya Tanzania John Pombe Magufuli aliwavutia wengi kwa tukio la kumpigia simu staa mkubwa Diamond Platnumz kipindi na ambapo alikuwa akitumbuiza stejini.
Katika tamasha kubwa lililofanyika Kigoma, msanii huyu alikuwa anasherehekea maadhimisho ya miaka 10 katika sanaa ya muziki.
Magufuli alipiga simu kupitia msemaji wa Chama Cha Mapinduzi Bwana Humphrey na kumsifia kuwa yeye ni mwanaume.
Katika mtandao wa Insta, Diamond amefunguka na kumsifia sana rais huyu.
"Ni adimu sana kumpata rais ambaye anaweza jali wananchi wake, akawajali vijana, tena hususan kujali wanasanaa...rais ambaye licha ya wingi wa majukumu mazito aliyonayo lakini akatenga muda kutazama onyesho lako.... kama haitoshi, katikati ya show akakupigia na simu juu kukupongeza kwa kazi uifanyayo.. lakini pia kuwasalimu na kuwatakia Kheri watu waliohudhuria show hio..." Alisema Diamond.