Akizungumza katika hafla ya kuchangisha pesa kwa wahudumu wa bodaboda mjini Webuye, Wamalwa amesema kuwa itakuwa vigumu kwa jamii ya Luhya kuungana na kuiongoza taifa hili iwapo viongozi wa eneo hilo watazidi kuwa katika vyama
tofauti.
Na kwa habari zingine;
Seneta wa Bungoma Moses Wetangula amemtaka rais Uhuru Kenyatta kuleta fedha za kuwalipa wakulima wa miwa bali si kuwapa wasimazi wa viwanda vya Nzoia na Mumias fedha ambazo wanafuja bila kudai masilai ya wakulima.
Wetangula ametaka usimamizi wa viwanda hivyo kubadilishwa akidai kwamba usimamizi mbaya ndio chanzo cha masaibu ya viwanda hivyo
Wetangula amesema kwamba kamati ya seneti inashughulikia jinsi wakulima wa maindi wameporwa mamilioni ya fedha kwa kuhakikisha walio pora fedha wanakabiliwa ipasavyo na sheria.
Brian O Ojama