Fake Money:Polisi wamsaka raia wa Cameroon baada ya mkewe kunaswa na Shilingi milioni 1 feki

Hamida Tabulo aliyekamatwa na shilingi milioni moja pesa bandia
Hamida Tabulo aliyekamatwa na shilingi milioni moja pesa bandia
Makachero huko Mombasa wanamsaka mwanamume mmoja raia wa Cameroon anayeaminika kuwa sehemu ya genge la wahalifu wanaotengeza pesa bandia  nhcini baada ya mkewe kukamatwa Bombolulu ,kaunti ndogo ya Nyali jumamosi usiku . Makachero walivamia nyumba ya mshukiwa  na kumkamata mwanamke kwa jina Mati Hamida Tabulo mwenye asili ya Kikenya na Tanzania pamoja na mfanyikazi wa nyumbani .

Kamanda wa polisi wa kaunti ndogo ya Nyali  Simon Thirikwa  amesema pesa hizo zina  noti za kale na mpya  .Hamida  anaripotiwa kuongoza  kundi la watu wanaochapisha pesa bandia linalohudumu Mombasa na Nairobi . Polisi sasa wanamsaka mumewe  aliyetoroka wakati wa oparesheni hiyo  na ambaye husimamiakanisa moja katika eneo la  Tudor na hujifanya kuwa raIa wa Congo . Raia mmoja wa Nigeria aliyekwepa mtego huo  pamoja na raia huyo wa Cameroon pia anasakwa. Ripoti za ujasusi zasema Hamida ambaye amepata ushawishi mkubwa kutokana na oparesheni zake ametumia kiasi kikubwa cha pesa alizo nazo kuwalinda wanachama wa genge lake dhidi ya kukamatwa .

Polisi pia wamemhusisha na ulaghai mkubwa wa kuwapunja watu fedha kwa kuwapa tiketi,visa na vibaki feki vya kufanyia kazi  na kuwahadaa kwamba wanawatafutia kazi katika mataifa ya mashariki ya kati . Januari mwaka huu polisi  walivunja  genge la uchapishaji wa pesa bandia  lenye uhusiano na wahalifu nchini marekani na kunasa  shilingi milioi 6.67  za noti za shilingi 1000  ambazo zilikuwa katika hatua za mwisho mwisho za kutengezwa katika nyumba  moja  huko Mtwapa .