Green light: Wana taaluma kutoka Ukambani waunga mkono Kalonzo kushirikiana na Jubilee

kalonzo
kalonzo
Kundi moja la  wanataaluma kutoka Ukambani  limeunga mkono hatua ya kiongozi wa chama cha wiper Kalonzo Musyoka  kufanya kazi na rais Uhuru Kenyatta na chama chake cha Jubilee.

Wamesema hatua hiyo italeta uoja na kuboresha ustawi wa kijamii na kiuchumi katika eneo la na kote nchini

Wanataaluma hao  ni pamoja na Daniel Yumbya  wa  Kenya Medical Practitioners and Dentists Council,  ambaye pia ni mwenyekiti wa  Kamba Professionals Forum .

Wengine ni  afisa mkuu mtendaji wa Kenya Film Classification Board Erick Mutua, mwenyekiti wa Kenya Medical Training College Philip Kaloki, Aliyekuwa  mwenyekiti wa  EACC Mumo Matemu  na mhadhiri wa chuo kikuu cha  Kenyatta Prof Donald Kombo,South Eastern Kenya University VC Prof Geoffrey Muluvi, aliyekuwa mkurugenzi wa  KMTC Dr Timothy King'ondu, Mkurugezi wa Ease of Doing Business John Mwendwa  na  Prof Julius Kyambi  wa chuo kikuu cha UoN .

Zaidi ya wanachama 50 wa  baraza kuu la chama cha Wiper  waliimpa Kalonzo Idhini ya  kukubali ushirikiano wa kufanya kazi na c vyama vya Jubilee na Kanu .

Baraza kuu la chama hicho  liliongeza kuwa pindi mkataba huo utakapoafiwa ,utatiwa saini na mwenyekiti wa chama  Chirau Ali Mwakwere  na katibu mkuu  Judith Sijeny.

Wanataaluma hao wamesema  wanaunga mkono kikamilifu ushirikiano hu kwa sababu maendeleo na siasa yanakwenda sako kwa bako .

Waliongeza kwamba tangu Kenya kujinyakulia uhuru ,eneo la ukambani limekuwa likipata tu maendeleo yafaayo kwa kushirikiana na serikali iliyo madarakani .