Habari za hivi sasa! Tuju ahusika katika ajali ya barabarani

tuju.2.jfif
tuju.2.jfif
Katibu mkuu wa Jubilee Raphael Tuju amehusika katika ajali ya barabrani na amekimbizwa katika hospital ya Kijabe.

Tuju ambaye alikuwa safarini kuhudhuria mazishi ya hayati rais mustaafu Danel Moi anatarajiwa kusafirishwa hadi Nairobi kwa uchunguzi zaidi.

Inasemekana gari alimokua akisafiria liligongana na matatu.

Ripoti hata hivyo zasema kwamba amepata majeraha madogo ingawa dereva wake amevunjika mkono katika ajali hiyo ya leo asubuhi.

Tutakuletea habari zaidi...