Mbunge wa Tiaty William Kamket amewashtumu polisi kwa kutochukua hatua za kumtafuta mwanafunzi wa chuo kikuu aliyetekwa nyara katika kituo cha kawi ya mvuke cha olkaria ambapo alikuwa akifanya masomo ya kujifunza kazi . Kamket amesema mwanafunzi huyo alitoweka jana usiku mjini Naivasha wakati alipokuwa akiburudika na wenzake na amemshtumu OCPD WA eneo hilo kwa kujikokota katika jitihada za kuwakamata washukiwa .
Upo katika hatari ya kuhusika katika ajali ya barabarani siku za ijumaa ,jumamosi na jumapili kuliko siku yoyote ya wiki .Takwimu za NTSA ZAONYESHA KWAMBA watu zaidi ya 400 waliaga dunia katika ajali zilizotokea katika siku hizo kati ya januri na oktoba . watu 500 waliaga dunia siku za jumapili ,480 siku ya jumamosi ilhali 406 waliaga dunia siku za ijumaa .
Shirika la feri limeikabidhi familia ya marehemu Mariam Kighenda shilingi laki mbili ili kuisaidia familia yake kwa matayarisho ya maazishi yake na bintiye Amanda Mutheu . mumewe Mariam , JoHN WAMBUA PIA amepokea hundi ya shilingi elfu 682,500 kutoka kwa kampuni ya bima kwa gari lao lilitumbukia baharini na familia yake
Kiongozi wa ANC Musalia Mudavadi amewaomba waajiri kuwaruhusu wafanyikazi wao wanaoishi Kibra kushiriki uchaguzi wa Novemba tarehe saba .Mudavadi amesema wenyeji wana wajibu wa kumchagua kiongozi ataayekamilisha kazi nzuri iliyoanzishwa na marehemu Ken Okoth .
Mzozo kati ya serikali na madreva wa magari ya mizigo unaendelea licha ya serikali kusema kwamba iliondoa agizo lililohitaji mizgo yote kusafirishwa kwa reli ya SGR .mfanyibiashara salim karama amesema hakuna kampuni ya uchukuzi iliyorejelea oparesheni zake .