Abby Cherop ,bintiye naibu wa rais William Ruto aliyezaliwa katika uhusiano wa pembeni amejiunga na kidato cha kwanza katika shule ya wasichana ya Alliance baada ya kupita mtihani wake wa KCPE kwa kupata alama 406 mwaka jana .
Katika picha zilizowekwa kwenye mitandao ya kijamii Abby alipelekwa shuleni na mamake Priscah Jemutai Bett, pamoja na jamaa zakekadhaa na walionekana katika kituo cha mabasi akiwa na bidhaa zake wa kwenda shule . Bintiye Ruto aliangaziwa kwa mara ya kwanza mwaka wa 2017 baada ya mamake Bett kumshtaki naibu w arias akitaka usaidizi wa kumlea .
Ruto alijitokeza na kukiri kwamba Abby alikuwa mwanawe na alikuwa akitunzwa vizuri kinyume na madai ya mamake . Wawili hao walikutana mwaka wa 2005 wakati Bett alipokuwa mwanafunzi katika chuo kikuu cha Moi na Abby akazaliwa mwaka wa 2006 .