Alifariki akiwa hospitali ya Eldoret, mwanafunzi huyo aliyefahamika kama Eliakim Oundo alipata majeraha hayo wakiwa wanacheza na timu mbili za raga za shule ya upili ya Sigalame na Nambale.
Eliakim alikuwa mwanafunzi wa shule ya upili ya Sigalame
Akiongea na stesheni moja humu nchini, babake Eliakim aliwalaumu walimu kwa kutochukuwa hatua za haraka kuhusiana na kitendo hicho baada ya timu ya Nambale kuwatishia wachezaji wa Sigalame kuwaumiza.
"Baadhi ya walimu wengine waliniambia kuwa timu ya Nambale walikuwa wametishia kuumiza na kufanyia kitendo timu ya SigalameWalisema kuwa ambyulensi inapaswa kuwa tayari kwa maana kuna mtu atakufa ama kuumia, najihisi kuwa usimamizi wa shule hii ungechukua hatua zaidi ili kubaini kiini cha matisho hayo
Baina ya timu hizo mbili." Alieleza.
Tukio hilo lilitokea ijumaa wiki jana, Eliakim alipelekwa katika hospitali ya Busia na kupelekwa tena katika hospitali ya kibinafsi ya Life Care kaunti ya Bungoma.