Watu 247 wapatikana na virusi vya corona

Akitoa taarifa ya kila siku kuhusiana na virusi vya corona ,katibu msimamizi katika wizara ya afya Rashid Aman amesema watu 247 waoatikana na virusi hivyo na kufikisha idadi nchini kuwa 7,188.

Watu 39 wameruhusiwa kuondoka hospitalini na kufikisha watu 2,149 waliopona.

Wagonjwa wawili wamefariki na kufikisha watu 154 waliofariki kutokana na virusi hivyo.

Kati ya visa hivyo vipya,wakenya ni 242 huku watu 5 wakiwa raia wa kigeni.

Wanaume ni 164 huku wanawake wakiwa 63,waathiriwa wakiwa kati ya miaka 1 na 100.

Nairobi imesajili visa 154 kati ya visa vipya vilivyosajili huku kaunti ya Mombasa ikiwa na watu 35.

Kaunti zingine zilizoathirika ni  Kajiado 15, Busia 12, Kiambu 12, Uasin Gishu 4, Machakos 4, Garissa 4, Murang’a 2, Nakuru 2, Siaya 2, Lamu 1, & Nyamira 1.

Wakati uo huo Aman amewataka wazazi kuwapeleka wasichana wa miaka 10 kupata chanjo ya HPV.

Visa vilivyosajiliwa katika kaunti ya Nairobi vimetokea maeneo, yafuatayo Kibra (35), Westlands (28), Dagoretti North (16), Kasarani (13), Embakasi East (12), Starehe (10), Langata (8), Makadara (6), Embakasi South (5), Embakasi West (4), Kamukunji (4), Roysambu (4), Dagoretti South (3), Ruaraka (3), & Embakasi Central (2).