Nendeni mkawatukane mama zenu ,muachane na wangu-Uhuru

uHURU
uHURU
Nendeni  mkawatukane mama zenu  na muachane na wangu ,rais Uhuru Kenyatta  amewajibu wanasiasa waliotoa matamshi ya kumshambulia aliyekuwa mama wa taifa  Mama  Ngina Kenyatta .

" Naelekea kukagua barabara moja hapa chini ambayo tunajenga na itaunganisha  Naiorbi  kupitia  Kiambu  hadi Murang’a kisha ifike Nyeri… niliwaambia mimi haja yangu ni kazi ..’ amesema rais

" Hata kama umri wangu ni mdogo  sina tatizo na kwenda nyumbani ili mradi watu waone kazi ambayo nimefanya . hawa wajinga  wanaozunguka wakitoa matusi  ,waambie watusi mama zao na waachane na wangu..’

Uhuru  ambaye alikuwa kizungumza kwa lugha ya kikuyu  amesema viongozi wanafaa kushirikiana kuleta umoja na Amani .

"..  Sitajiruhusu kuzungumza kwa hamaki kwa sababu nawataka wakenya kuishi pamoja kwa Amani’

" taifa litasalia kuwepo lakini sisi kama watu hatutaishi milele’

Matamshi hayo ya rais yanajiri baada ya mbunge wa Emurua Dikiir Johanna Ng’eno na wa kapsrete Oscar Sudi  kurekodiwa wakizingumza matamshi ambayo  yalionekana kumlenga rais Kenyatta na familia yake . Ng;eno baadaye alikamatwa na ameachiliwa leo na mahakama kwa dhamana ya shilingi milioni 1

Baadhi ya viongozi wamejitokeza kutoa onyo dhidi ya mtindo wa kutumia lugha mbaya nay a uchochezi inayotishia Amani ya nchi kabla ya uchaguzi mkuu wa 2022