Oparanya ataka serikali kukomesha usajili wa NHIF na kushauriana na magavana

Muhtasari

• Oparanya  amesema serikali za kaunti zinafaa kushauriwa kuhusu usajili

• Ameongeza kwamba  utekelezaji wa UHC ni jukumu la serikali kuu na za kaunti 

Oparanya
Oparanya

Mwenyekiti wa baraza la magavana Wycliffe  Oparanya ameitaka wizara ya  afya kukomesha usajili unaoendela wa NHIF katika kaunti .

 Hii  ni baada ya kaunti kugundua kwamba usajili huo unaendeshw akatika kaunti zao bila magavana kujulishwa .

 
 

 Mojawapo ya ajenda kuu za rais Uhuru Kenyatta ni utekelezwaji wa mpango wa kutoa huduma za bure za matibabu kwa wananchi wote .

 Mpango huo wa UHC sio tu jukumu la serikali kuu bali unafaa kutekelezwa kwa ushirikiano na  serikali za kaunti .

 “ Komesheni mpango huo wa usajili wa NHIF… kukosa kushauriana nasi na uksoefu wa uwazi katika usajili huo  ni jambo ambalo litazaa kutoaminiana’ Oparanya amesema

 Kupitia taarifa siku ya jumanne Oparanya amesema  usajili wa NHIF katika kaunti haufai kufanywa bila kauinti kuhusishwa.

" Utaratibu  huo muhimu unafaa kufanywa  na vitengo vyote vya serikali baada ya kukubaliana kuhusu jinsi ya kuendesha usajili huo na namna ambavyo mradi mima wa UHC utakavyofanikishwa’ ameongeza.