- Sonko alisema kwamba hataachili pesa zozote mpaka pale NMS itahalalishwa
- Gavana huyo aloisema kwamba afungwe lakini kuna maisha baada ya kufungwa na kifo
Gavana wa kaunti ya Nairobi Mike Sonko kupitia kwenye ukurasa wake wa twitter amesema kwamba hatakubali vitisho vya wapinzani wa kisiasa.
Pia Sonko alisema kwamba yuko karibu kukufa kwa ajili ya kushikilia katiba ya kenya kwa kufanya kazi ambayo inastahili katika sekta yake.
Pia alisema kwamba hataachilia fedha ili kumpa bosi wA NMS kwa maana ni kinyume cha sheria na katiba.
" Nina suluhisho za kupendeza lakini nini haswa hutendeka tunapokutana katia mkutano ili kutoa suluhisho hizi ndiposa wakazi wa Nairobi wapate huduma nzuri huwa tunatofautiana katika sheria kina chofuata ni vitisho
Siku za gia zimepita sitamkubali mtu kunitishia kwa ajili ya sheria, wacha tufuate sheria na kisha wahalalishe NMS nitaachilia pesa." Sonko aliongea.
Jail me! There's life in prison. Impeach me! There's life after politics. Kill me! There's life after death where my late father and our beloved founding father of the Republic of Kenya the late Mzee Jomo Kenyatta are resting in peace. But there's no amount of intimidation.. pic.twitter.com/iKHnWhhKzr
— Mike Sonko (@MikeSonko) November 16, 2020
Sonko alikuwa mbele ya kamati ya seneti ili kujibu maswali kuhusu kuachilia kwa fedha hizo.
"Nifungeni jela, kuna maisha baada ya siasa, niueni lakini bado kuna maisha baada ya kifo ambapo mwendazake baba yangu, mababu wa nchi yetu kama mzee Jomo Kenyatta wamelala kwa amani lakini hakuna kiasi cha vitisho." Sonko Alizungumza.