Tunashukuru shule ambazo zinahakikisha ya kwamba wanafunzi wanaendelea na kupokea masomo wakati huu." Aliongea Magoha.
Waziri alisema kwamba wizara hiyo ina furaha tele baada ya asilimia 80 ya wanafunzi kurejea shuleni
Magoha alisema kuwa serikali imetoa madawati yakutosha ili kuhakikisha wanafunzi wamesoma bila tashwishwi yeyote.
Pia alionya walimu wakuu wa shule dhidi ya kuwatuma wanafunzi nyumbani kwa ajili ya karo ya shule, huku akiwaamia wanapaswa kuelewa jinsi uchumi umekuwa mbaya kwa ajili ya janga la corona.
Shule zilifungwa rasmi mwezi wa machi 2020 baada ya kisa cha kwanza cha virusi vya corona kuripotiwa nchini.
"Kwa shule za msingi na sekondari hatupaswi kuwa na mjadala kwa ajili ya karo,kwa maana serikali tayari imetoa pesa kwa mashule, hakuna mwanafunzi anapaswa kurudishwa nyumbani."