Shule kufunguliwa kulingana na kalenda-Uhuru Kenyatta

Muhtasari
  • Makanisa yaliagizwa kushikilia ibada ya kibinafsi na kuzingatia kanuni za wizara ya afya

Rais Uhuru Kenyatta siku ya sikukuu ya Labour Day amesema shule zinapaswa kufunguliwa Mei 10 kama ilivyoratibiwa kwa kalenda ya wizara ya elimu.

Makanisa yaliagizwa kushikilia ibada ya kibinafsi na kuzingatia kanuni za wizara ya afya.

Hata hivyo, alionya kuwa ni muhimu kwa Wakenya kuelewa kwamba kulinda watoto wa shule ni kipaumbele kwa wote na Kenya

"Katika kipindi hiki cha kufungua shule, wacha tuwe raia wenye heshima na wazalendo wa ardhi yetu. Hakuna mtu anayefurahia hali tuliyomo. Hatufurahi kuwaweka Wakenya katika wakati mgumu.

"Lakini ikiwa hatuwezi kudhibiti ugonjwa huo kwa sababu ya ubinafsi wetu, basi tutarudisha na kulinda maisha. Tutalazimika kulinda maisha na uchumi. Ikiwa tutafanya kazi pamoja kama Wakenya tutaweza kuendelea na maisha kama kawaida iwezekanavyo, "Uhuru alisema.

Rais pia aliagiza migahawwa kufunguliwa kuanzia saa moja asubuhi hadi saa moja usiku.