Balozi wa Italia auawa katika shambulio DRC

crime scene 1
crime scene 1

Wizara ya mambo ya nje ya Italia imesema kuwa balozi wake nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo ameuawa katika shambulio dhidi ya msafara wa magari ya Umoja wa Mataifa mashariki mwa nchi hiyo.

Balozi Luca Attanasio na mwanajeshi mmoja wa Italia wameuawa katika shambulio lililotokea karibu na mji wa Kanyamahoro.

Maafisa katika mbuga ya wanyama ya Virunga wanasema shambulio hilo lilikuwa jaribio la utekaji nyara.

Makundi mengi yaliyojihami yanaendesha harakati zake karibu na mbuga hiyo inayopakana na Rwanda na Uganda.

Walinzi wa mbuga hiyo wamekuwa wakishambuliwa mara kwa mara na kuuawa na waasi.