Rais wa kwanza wa Zambia afariki akiwa na miaka 97

Muhtasari
  • Mmoja ya watu maarufu zaidi barani Afrika na mpiganiaji uhuru, Kenneth Kaunda ameaga dunia nchini Zambia akiwa na umri wa miaka 97

Mmoja ya watu maarufu zaidi barani Afrika na mpiganiaji uhuru, Kenneth Kaunda ameaga dunia nchini Zambia akiwa na umri wa miaka 97.

Kaunda maarufu kama KK alikuwa rais wa kwanza wa Zambia huru.

Alikimbizwa katika hospitai moja mjini Lusaka mapema wiki hii na kulazwa baada ya kuugua homa ya mapafu.

Mwaka 1950 , bwana Kaunda alikuwa mtu muhimu katika Vuguvu la kupigania uhuru wa Rhodesia ya kaskazini kutoka kwa Uingereza.

Nahuzunika kusema kwamba tumempoteza Mzee', mwana wa Kaunda Kambarage , aliandika katika ukurusa wa facebook wa babake akiwataka wafuasi wake kumuombea babake.

Rais wa Zambia Edgar Lungu amesema kwamba taifa hilo lilikuwa likimuomboleza mtoto mwa wa Afrika.

''Niligundua kwamba umefariki leo mchana nikiwa na majonzi makubwa'', aliandika katika facebook.

'Kwa niaba ya taifa lote na kwa niaba yangu naomba kwamba familia yote ya Kaunda inafarijika wakati tunapomuomboleza rais wetu wa kwanza na mwana wa Africa'''.

Kalusha Bwalya, nahodha wa zamani wa timu ya taifa ya Zambia amesema kwamba Kaunda amefanya mengi nchini humo. "

Alikuwa Rais wa kwanza wa Zambia mwaka 1964 na kuongoza taifa hilo kupitia miongo kadhaa ya utawala wa chama kimoja.

Alijiuzulu baada ya kupoteza katika uchaguzi wa vyama vingi 1991.

Bwana Kaunda alikuwa shabiki mkubwa wa juhudi za kumaliza ubaguzi wa rangi nchini Afrika Kusini.

Alikuwa pia akiongoza mavuguvugu nchini Msumbiji na nchini Zimbabwe.