Marekani kuilinda Taiwan iwapo China itaishambulia

Biden asema Marekani itailinda Taiwan iwapo China itaishambulia

Muhtasari

'Tutailinda Taiwan China ikianza mashambulizi'-Biden

Marekani kwa muda mrefu imekuwa ikifanya "utata wa kimkakati" linapokuja suala mwiba wa kutetea Taiwan.

Image: GETTY IMAGES

Rais wa Marekani Joe Biden amesema nchi yake itatetea Taiwan ikiwa Uchina itashambulia, hatua ambayo inatofautiana hadharani na sera ya muda muda mrefu ya Marekani

"Ndio, tuna wajibu wa kufanya hivyo," alisema alipoulizwa katika ukumbi wa mji alipoulizwa iwapo Marekani itailinda Taiwan .

Lakini msemaji wa Ikulu baadaye aliambia baadhi ya vyombo vya habari vya Marekani kwamba matamshi yake hayakuashiria mabadiliko ya sera.

Marekani kwa muda mrefu imekuwa ikifanya "utata wa kimkakati" linapokuja suala mwiba wa kutetea Taiwan.

Hii inamaanisha kuwa Marekani imekuwa na msimamo wenye utata kwa makusudi juu ya kile itakachofanya ikiwa China itashambulia kisiwa hicho.

Marekani haina uhusiano wowote wa kidiplomasia na Taiwan, lakini inauza silaha kwa kisiwa hicho kama sehemu ya Sheria ya Uhusiano ya Taiwan, ambayo inasema kuwa Amerika lazima isaidie Taiwan kujilinda .

China inaona Taiwan kama jimbo lililojitenga, ambalo linaweza kuchukuliwa tena kwa nguvu siku moja ikiwa ni lazima, wakati Taiwan inadai kuwa ni nchi huru.

Mvutano umekuwa ukiongezeka kati ya nchi hizo mbili katika wiki za hivi karibuni baada ya Beijing kurusha ndege kadhaa za kivita katika eneo la ulinzi wa anga la Taiwan.

Utawala wa Rais Joe Biden uliidhinisha mauzo mengine ya kibiashara ya moja kwa moja kwa Taiwan tangu achukue madaraka mapema 2021, na imetaka kuimarisha uhusiano zaidi na kisiwa hicho, na kusababisha hasira kutoka Beijing.