Mzozo wa Ukraine : Ujerumani yasitisha bomba huku nchi nyingi zikiiwekea Urusi vikwazo

Muhtasari

• Siku ya Jumatatu rais wa Urusi alitambua mikoa miwili iliyojitenga ya Ukraine kama nchi huru

• Putin aliamuru wanajeshi wa Urusi kutumwa kwa nchi zote mbili.

• Ujerumani ilisitisha uidhinishaji wa bomba la Nord Stream 2 na mataifa mengine ya Magharibi yakatoa vikwazo.

Image: EPA

Ujerumani imesimamisha bomba kuu la gesi la Urusi kufuatia agizo la Vladimir Putin la kutuma wanajeshi nchini Ukraine.

Siku ya Jumatatu rais wa Urusi alitambua mikoa miwili iliyojitenga ya Ukraine kama nchi huru na kuamuru wanajeshi wa Urusi kutumwa kwa nchi zote mbili.

Mataifa ya Magharibi kwa kiasi kikubwa yanaona hatua hiyo kama kisingizio cha uvamizi mpana.

Kwa kujibu, Ujerumani ilisitisha uidhinishaji wa bomba la Nord Stream 2 na mataifa mengine ya Magharibi yakatoa vikwazo.

Vikwazo vinaweza kuchukua aina mbalimbali - neno hilo linaweza kurejelea vitendo vingi vinavyotumiwa na nchi moja kudhuru nchi nyingine, kwa kawaida kuzuia vitendo vikali au ukiukaji wa sheria za kimataifa.

Bomba la Nord Stream 2 limeungwa mkono na Ujerumani licha ya upinzani kutoka kwa nchi kama vile Marekani, Uingereza, Poland na Ukraine. Iligharimu €10bn (£8.4bn), huku ufadhili ukigawanyika kati ya makampuni ya nishati ya Urusi na nchi za Magharibi.

Lakini kufuatia agizo la Bw Putin la kutuma wanajeshi katika mikoa ya Ukraine inayoshikiliwa na waasi ya Donetsk na Luhansk, Ujerumani ilitangaza kuwa inasitisha mchakato wa kutoa leseni ya bomba kati yake na Urusi na uendeshaji - na hivyo kusimamisha mradi huo .

Hatua hiyo ni kubwa kwani Urusi inaipatia Ulaya karibu 40% ya gesi yake, inayopatikana kutoka kwa usambazaji mkubwa mashariki mwa Urusi.

"Hii ni hatua ya kimaadili, kisiasa na kivitendo sahihi katika hali ya sasa," Waziri wa Mambo ya Nje wa Ukraine Dmytro Kuleba aliandika, akiukaribisha uamuzi huo. "Uongozi wa kweli unamaanisha maamuzi magumu katika nyakati ngumu. Hatua ya Ujerumani inathibitisha hilo."