Nitawashinda baada ya baba yangu kustaafu, mwanawe Museveni aonya upinzani

Muhoozi amezua mjadala mpya nchini Uganda kwa kudai kuwa ndiye rais anayefuata wa nchi hiyo.

Muhtasari

•Muhoozi alionyesha imani kuwa upinzani chini ya mwanamuziki aliyegeuka mwanasiasa Robert Kyagulanyi almaarufu Bobi Wine hautawahi kuongoza nchi baada ya kustaafu kwa babake.

•Mnamo Mei 2019, Muhoozi alichapisha meme inayoonyesha jinsi yeye na 'kaka yake' walivyokuwa waking’ang’ania  nafasi hiyo.

KWA HISANI
KWA HISANI
Image: Muhoozi Kainerugaba

Mtoto wa Rais Yoweri Museveni Muhoozi Kainerugaba amezua mjadala mpya nchini Uganda kwa kudai kuwa ndiye rais anayefuata wa nchi hiyo.

Muhoozi alionyesha imani kuwa upinzani chini ya mwanamuziki aliyegeuka mwanasiasa Robert Kyagulanyi almaarufu Bobi Wine hautawahi kuongoza nchi baada ya kustaafu kwa babake.

"Kwa upinzani wa Uganda, baada ya baba yangu, nitawashinda vibaya katika uchaguzi wowote. Waganda wananipenda zaidi kuliko watakavyowahi kuwapenda," alisema kupitia Twitter siku ya Ijumaa.

Uganda ifanya uchaguzi mwaka wa 2026 kumchagua rais mpya. Museveni ameiongoza nchi hiyo tangu alipoingia madarakani mwaka 1978.

Bobi Wine, kiongozi wa National Unity Platform, alitangaza azma yake ya urais kwa mara ya kwanza mwaka wa 2019 lakini akashindwa na Museveni katika uchaguzi wa 2021.

Hii si mara ya kwanza kwa Muhoozi kutoa maoni kuhusu mrithi wa urais.

 Mnamo Mei 2019, Muhoozi alichapisha meme inayoonyesha jinsi yeye na 'kaka yake' walivyokuwa waking’ang’ania  nafasi hiyo.

Aliandika, "Mimi na kaka yangu mdogo Kabobi tukibishana kuhusu nani anaweza kujaza viatu vya baba yangu! Shukrani kwa msanii bora nchini Uganda."

Akijibu tweet hiyo Bobi Wine alisema mimi sio kaka yako na wala sishindani na viatu vya baba yako, unastahili viatu vya M7, ng'ombe na hata kofia yake, kosa moja unalofanya ni kudhani Uganda ndio moja ya mali za baba yako ili urithi."

Kiongozi huyo wa upinzani siku za nyuma alidai kuwa Museveni alikuwa akimtayarisha Muhoozi kuwania kiti hicho, kwa nia ya kutaka kumpata mfalme.

Katika jibu la tweet ya Muhoozi siku ya Ijumaa, mtumizi wa Twitter aliuliza ikiwa kwa maneno "baada ya baba yangu", alimaanisha kuitambulisha Uganda kama eneo la ufalme.

"Chochote unachotuita. Uganda kamwe haitakuwa mali ya ukoloni mamboleo," Muhoozi alisema.