- Orodha ya wacheshi wanawake wanaovaa vizuri na wenye maridadi zaidi
Kuwa mashuhuri hasa kama wewe ni mwanamke ni jambo ngumu, kwani wanaume wamepewa fursa kubwa katika mitandao ya kijamii kuliko wanawake.
Licha ya changamoto ambazo baadhi ya wanawake mashuhuri hupitia wametia bidii katika kazi yao.
Katika makala haya tutazingatia wacheshi wanawake ambao wanavaa vyema na wenye maridadi zaidi nchini kenya.
1.Nasra
Ni mwanamke wa kiislamu ambaye amekuwa akitia bidii katika tasnia ya burudani, na mwenye mitindo ya kipekee.
2.Awinja
Ni mcheshi ambaye alifahamika sana kupitia kwenye kipindi cha papa Shirandula, bali na uigizaji wake, amekuwa akiwafurahisha mashabiki wake kupitia kwenye mitandao yake ya kijamii.
3,Cartoon Comedian
Licha ya changamoto ambazo amepitia kwenye tasnia ya burudani, mcheshi huyo ni miongoni mwa wacheshi bora nchini na wenye mitindo ya kipekee.
4.Mammito
Kupitia kwa video zake ambazo hupakia kwenye mitandao ya kijamii Mammito amezidi kutia bidii kwenye kazi yake ya ucheshi.
5.Zeddy
Alifahamika sana kupitia kwenye kipindi cha Churchill na amekuwa mfano mwema kwa wacheshi wenzake na mwenye mavazi mazuri.