- Haya yanajiri saa chhache baada ya msemaji wa Azimio Makau Mutua Katika taarifa alisema Winnie ni mwanasiasa mchanga na anafaa kuelimishwa
Winnie Odinga amevunja kimya na kusema hakuna binadamu anayestahili kumhukumu.
Katika taarifa yake Jumatano, Winnie alijitetea dhidi ya shutuma kwamba alihujumu timu ya Azimio la Umoja wakati wa uchaguzi mkuu wa Agosti 9.
"Yule ambaye amejichanganya katika msukosuko wa wajibu ambao wajasiri hustahimili, lazima atakuwa amefanya maadui. Ikiwa huna, kazi ambayo umefanya ni ndogo. Hujawahi kugeuza kosa kuwa sawa. Umekuwa mwoga katika vita."
Charles Mackay
Ni Mungu pekee ndiye anayeujua moyo wangu, atanihukumu tu,"Winnie Aliandika.
Haya yanajiri saa chhache baada ya msemaji wa Azimio Makau Mutua Katika taarifa alisema Winnie ni mwanasiasa mchanga na anafaa kuelimishwa.
"Wale ambao wamekuwa wakimshambulia Winnie Odinga wakome na waache. Yeye ni mwanamke mchanga katika siasa. Mwanamume amabye yuko kwenye hali yake hatakuwa mjanja sana. Winnie alipata talanta, lakini ushauri utakuwa muhimu. Tuwaunge mkono vijana wetu," Mutua alisema.
Winnie alirejea kwenye mitandao ya Twitter baada ya mwezi mmoja wa kuzima mtandao huo.
"He who has mingled in the fray of duty that the brave endure, must have made foes. If you have none, small is the work that you have done. You’ve never turned the wrong to right. You’ve been a coward in the fight."
— WinnieOdinga (@Winnie_Odinga) October 19, 2022
Charles Mackay
Only God knows my heart, only he will judge me. pic.twitter.com/e6ucPZxpAA