Familia ya maajabu: Mama amkubalia mumewe kuoa binti yao wa damu kwa kuzaa naye

Mama huyo alijuta kwa kwenda mbali kazini kwa muda mrefu na kumuacha mumewe na binti yake jambo lililootesha mzizi wa mapenzi kati yao.

Muhtasari

• “Alitaka kumpeleka mumewe jela kwa kumlazimisha binti yao kulala naye na kupata mtoto naye lakini akagundua hilo halikuwa suluhu,” Afrimax waliripoti.

• Binti huyo pia alijuta sana kufanya mapenzi na baba yake lakini majuto hayo hayangeweza kubadili kitu.

Mama amruhusu mumewe kuoa binti yake baada ya kuzaa naye
Mama amruhusu mumewe kuoa binti yake baada ya kuzaa naye
Image: Screengrab//YouTube

Mama mmoja amesimulia kwa machungu yaliyopitiliza jinsi alikwenda kazini kwa muda na aliporudi nyumbani alipata binti yake amesha zaa na baba yake ambaye ni mumewe.

Katika Makala mafupi yaliyopeperushwa na chaneli ya Afrimax, mama huyo baada ya kupata matukio hayo nyumbani kwake, alishindwa cha kufanya na jawabu pekee lililosalia kwake ni kukubali matokeo na kuwasamehe, hivyo kukubali kuishi na binti yake kama mke mwenza.

Kwa mujibu wa Makala hayo, mama huyo aliumia sana na nusra aitake talaka yake, lakini alipata wazo kwamba hilo halingeweza kusuluhisha mambo na badala yake lingepata mbegu ya uadui miongoni mwao, achia mbali kumkaribisha shetani kwenye familia.

“Alitaka kumpeleka mumewe jela kwa kumlazimisha binti yao kulala naye na kupata mtoto naye lakini akagundua hilo halikuwa suluhu,” Afrimax waliripoti.

Binti huyo pia alijuta sana kufanya mapenzi na baba yake lakini majuto hayo hayangeweza kubadili msimamo na ukweli wa matukio kuwa alikuwa ameshazaa mtoto na baba.

“Mama huyo baada ya kujirudi aligundua ni makosa yake kwa kumuacha mumewe kwa muda mrefu, jambo lililootesha hisia za kujamiiana kwa bintiye. Hapo aliamua kusamehe na sasa wote wanaishi maisha mazuri kama familia ya mitala,” Makala hayo yalisema.

Licha ya changamoto hizo za picha za kutukanisha familia, waliamua kuzika tofauti na kuja pamoja kukubaliana na kilichotokea kwani siku zote wenye midomo walisema kitanda hakizai haramu.

Ama kweli, adhabu au hata kifungo jela hakimfanyi mtu kuwa mwema ila kujuta na kukiri makosa na kuomba msamaha kutoka kwenye shina la moyo, hufanya.